Next
Previous
Showing posts with label Ommy Dimpoz. Show all posts

Sunday, August 11, 2013

0

NABII HAKUBALIKI KWAO: ONA JINSI OMMY DIMPOZ ALIVYOPOKELEWA BURUNDI

Posted in
ommy


Ommy Dimpoz licha ya kukwama kwa muda kidogo kwenye Airport ya Jomo Kenyatta, hatimaye aliweza kufika nchini Burundi na kufanya show. Baada ya kufika Burundi,  njiani kuelekea kwenye show Ommy Dimpoz alifuatwa na kundi kubwa la watu wakifuatilia gari lake huku yeye akiwapungia mkono. Cheki hii picha kutoka kwake mwenyewe Ommy Dimpoz

Thursday, August 1, 2013

0

HII NDO NYIMBO MPYA YA DIMPOZ, ALIYOFANYA NA J.MARTINS | OMMY DIMPOZ FT. J.MARTINS - TUPOGO

Posted in ,

Sunday, July 21, 2013

0

PHOTOS: WEMA SEPETU AKIFUTURISHA NYUMBANI KWAKE

Posted in ,
WEMAAFUTURU3
Mrembo anayetamba kwenye filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ au Madam jana alifuturu pamoja na wageni wake nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waliofuturu pamoja na Wema ni pamoja na Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, Petit Man ‘Wakuache’ na wengineo.
WEMAAFUTURU4

Wednesday, July 10, 2013

0

OMMY DIMPOZ FT. J. MARTINS - TUPOGO (PROD. MARCO CHALI & MAN WATER)

Posted in ,


Mkali wa ngoma BAADAE, ME N YOU … Ommy Dimpoz anatarajia kuachia ngoma yake nyingine mwezi huu … Ommy ambae mwaka huu amefanya shows nyingi na bado anafanya ndani na nje ya nchi …

Akiwa pia amechukua tuzo kadhaa kwenye KTMA2013 ataachia ngoma hiyo mwezi huu ambayo ameshirikiana na J.MARTINS kutoka Nigeria …. Mzigo umetengenezwa MJ RECORDS na Marco Chali na Man Water (Combination Sound) …

Ngoma hiyo itafahamika kama TUPOGO …

Wednesday, June 26, 2013

0

OMMY DIMPOZ ASAINI MKATABA TOUR YA USA NA CANADA

Posted in

Omary Fereji Nyembo a.k.a Ommy Dimpoz, amesaini mkataba na kampuni ya DMK Global Promotion leo  hii kwa ajili ya tour atakayoifanya Canada na Marekani mwezi wa tisa mwaka huu.


"yaah nimesaini mkataba na nitaondoka kwenda kwenye tour hiyo mwanzoni mwa mwezi wa tisa, imekuwa hivyo kwasababu tunasubiri mwezi mtukufu upite si unajua tena, kampuni niliyosaini nayo inaitwa DMK global promotion ambayo ni ya mtanzania ambae anaishi marekani." amesema Dimpoz

nilipomuuliza kuhu mkwanja alioingiza kwa mkataba huo, Dimpoz aligoma kutaja kiasi na kusema
"aaaah unajua tena kwa matatizo yaliyotokea nikitaja tena na mkwanja nilioingiza si ndio itakuwa matatizo kabisa? .

Saturday, June 22, 2013

0

"NAI NAI" USA TOUR (OMMY DIMPOZ LIVE IN THE USA)

Posted in ,

Saturday, June 15, 2013

0

KUTOKA FACEBOOK: TID AAPA KUMKUNG'UTA OMMY DIMPOZ

Posted in ,


Hawa watoto wadogo wanakuja na kandambili kuomba kuimba sasa hivi wanajifanya wao wanazo hela sana na kututusi sisi especially mkali wangu Albert wallahi mungu
atamlaani.........mshenzi mkubwa na nikikuona nakupiga.
"Hicho ndicho alochokiandika TID aka mnyama kwenye kupitia ukurasa wake wa facebook"

Friday, June 14, 2013

0

OMMY DIMPOZ ASEMA HII NDO SABABU ILIYOFANYA NICHAFULIWE GAZETINI

Posted in ,
gazetiMapema leo hii, kimeonekana kichwa cha habari katika moja ya magazeti ya udaku kikiongelea OMMY DIMPOZ kumkashifu/kumtusi marehemu ALBERT MANGWEA [R.I.P] … Baadae kidogo Ommy Dimpoz aliandika mtandaoni kuwa si kweli na ni story ya kutunga tu kutaka kumchafua kisanii … Ommy, “Nimesikitishwa sana na hii habari iliyotoka global publishers Wanatengeneza story ili wauze magazeti yao” … alimaliza Dimpoz na kutupia picha hii hapa …

Lakini Ommy hakuishia hapo, alionesha kukerwa zaidi na front page hiyo na kuandika sababu ya gazeti hilo kumchafua namna hiyo …

Hichi ndicho Ommy alichoandika … “Nilipigiwa simu ya kibiashara kwa ajili ya kufanya show na global publishers kwa sababu hatukuafikiana kwenye malipo ndo wameamua kunichafua ..”

Sunday, June 2, 2013

0

MISS TABORA AIBU TUPU: MAKALIO YAANIKWA MBELE YA WABUNGE

Posted in

Mmoja wa washabiki wa muziki wa kizazi kipya ambaye alivaa vazi lililoacha  matako  nje....

Shabiki huyo  alipanda jukwaani kumkumbatia  msanii  maarufu nchini , Ommy Dimpoz  wakati alipokuwa akitoa burudani katika mashindano ya Redds Miss Tabora.

Tukio hilo la aibu lilitokea  mbele ya  wabunge....
Mbunge wa Jimbo la Sengerema  Bw.William Ngereja akiwa na Diwani wa kata ya Kitete manispaa ya Tabora Bw.Daniel Mhina ambaye alikuwa MC katika onesho hilo lililofanyika katika ukumbi wa Frankman Hotel mjini Tabora.
Ommy Dimpoz akitokwa na machozi wakati akitumbuiza jukwaani alipofikia hatua ya kumkumbuka marehemu msanii  maarufu Mangwea.
Ommy Dimpoz alionesha kukubalika zaidi katika onesho hilo
Mbunge Ngereja akiwa na mbunge wa vitimaalum mkoani Tabora wakijaribu kucheza kwa pamoja muziki uliokuwa ukiimbwa na Ommy Dimpoz.

Redds Miss Tabora 2013 Annastazia Donald(19)ambaye ni mwanafunzi wa Theofil Kisanji University,kushoto ni mshindi wa pili katika kinyang'anyiro hicho  Sabrina Juma(18) kutoka chuo cha African Utalii na mshindi wa tatu ni Cornecia Cossei(21)kutoka chuo cha Utumishi wa Umma Tabora.  

Monday, May 6, 2013

0

HUYU NDO MSANII WA KWANZA KUMUUNGA MKONO LADY JAY DEE KATIKA SAKATA LAKE NA CLOUDS

Posted in , , , , ,
Mkali wa miondoko ya bongo fleva anatamba na ngoma yake kali aliyomshirikisha OMMY DIMPOZI  chukua tyme SUMA MNAZALETI ameyasema maneno hayo leo kwa njia ya masseji Alisema'' ebana nadhani unajua nini kinaendelea kuhusu lady jaydee! nachukua nafasi hii we kaka yangu ambaye umenisaidia sana kwa mda mrefu kukujulisha kuwa mdogo wako,Nitakuwa msanii miongoni mwa wasanii wanao support maneno ya lady jay dee Nakwambia haya kwasababu najua umenisaidia sana,but kama baada ya haya utaamua kuona sifai  sio tatizo pia! no interview 4 NOW  Nilikuwa nakupa habari  kama ndugu yangu wa karibu. lakini kama hili unaliunga mkono sio mbaya ukinijulisha kwamba hakuna tatizo na unaendelea kusaport kazi zangu. alimaliza kwakuandika jina lake suma mnazaleti.

Tuesday, April 30, 2013

0

PICHA: OMMY DIMPOZ NA CHEGGE WAKIWA KWENYE ZIARA BARANI ULAYA

Posted in ,

Wednesday, February 6, 2013

0

OMMY DIMPOZ NA VANESSA KUZINDUA VIDEO YA ''me N you'' @NEW MAISHA CLUB

Posted in ,

Msanii Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa anatamba na track yake ya ''Me n You'' ambayo ameshirikiana na mwanadada Vanessa Mdee na ngoma hiyo kutokea kupendwa sana na watu wa rika karibu zote nchini hata nje pia.
Sasa habari mpya kuhusu ngoma hiyo ni kuwa Video ipo tayari na itaachiwa kwa mara ya kwanza katika ukumbi wa disco wa New Maisha Club ulioko maeneo Oysterbay jijini Dar siku ya Jumapili ya tarehe 10 mwezi huu.

Sunday, December 30, 2012

0

YALIYOJIRI 2012 KATIKA SANAA YA MUZIKI BONGO

Posted in , , , , , , ,

Muziki wa bogno umepiga hatua kubwa sana hasa katika mwaka huu. Mengi Yametokea, Vipaji vingi vimejitokeza. Mitindo mingi ya Kimziki na Dansi iliongezeka.

1. Kupaa Kwa Ommy Dimpoz
Pooooz kwa Poz...
Ommy Dimpoz Na Vanessa Mdee
Huu ulikua ni mwaka wa kijana huyu ambaye alianza kwa kutoka na Nyimbo NAI NAI iliyompa tuzo za kili kwa kumshirikisha Ally Kiba, Akaja na BAADAE, na baadae akafunga mwaka kwa nyimbo ya  ME & YOU ft. Vanessa Mdee. Kijana huyu ameepata mafanikio mengi na kupiga hatua moja ikiwa ni kufanya video nchini Afrika Kusini. Kijana huyu pia alitoa malalamiko ya kumshutumu Lord Eyez kuiba PowerWindow za Gari Lake(Rav4).



2. Kuendelea Kuvuma kwa WEUSI.
WEUSI ni Kundi Muanganiko wa wasanii wa Arusha toka kundi la N2N na RiverCamp likijumuisha Wasanii kama Lord Eyez, Joh Makini, G-Nako, Nikki Wa pili na Bonta. Kundi hili limekua na mafanikio mengi huku kashfa aliyoipata Lord Eyez, kulifanya lipate sifa mbaya na wale walioamini hilo.






3. Udhamini wa OSTAZ JUMA NAMUSOMA kwa WATANASHATI
Watanashati wamevuma sana katika mwaka huu, Wamemrudisha PnC katika Fani, Wameokoa kipaji cha Dogo Janja, Suma Mnazaleti kwa udhamini mzuri walionao. Kundi hilo lilizidi kuwa kubwa kadri mda ulivyokwenda, na wamevuma zaidi kwa nyimbo zao. Uwepo wa Marehemu Sharo Millionea na Teja Kitale uliweka uamsho katika kundi.
HONGERA OSTAZ JUMA


Tuesday, December 4, 2012

0

DOWNLOAD: DULLY SYKES FT. OMMY DIMPOZ & DIAMOND( TRIPLE D) -UTAMU

Posted in , ,
 
Download Track hii, Na utoe comments nani kamfunika mwenzake???
Brand new track from Dully Sykes

Sunday, November 11, 2012

0

VIDEO YA LORD EYEZ akizungumza na waandishi wa habari!! TUIPE MAHAKAMA MUDA, NAAMINI NTAPATA HAKI YANGU

Posted in , ,

Rapper wa kundi la Weusi, Lord Eyez amewataka wananchi kuiachia mahakama iamue hatma yake na kujizuia kumuita mhalifu kwakuwa bado chombo hicho cha sheria hakijatoa maamuzi yake.
Rapper huyo ametoa wito huo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa hoteli ya Double View iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
Lord Eyez alikuwa ameambatana na mwanasheria wake Peter Kibatala pamoja na members wenzie wa Weusi, Nikki wa Pili na G-Nako.
“Naomba tuipe muda mahakama naamini ntapata haki yangu na uhakika Mungu yuko pamoja nami na mafans wangu poleni sana naomba mnipe nafasi yenu nipate haki yangu niendelee kulisha madini sababu ninayo mengi lakini nimekuwa na misukosuko mingi ambayo Mungu pekee ndio anaweza kujua ukweli,” alisema Lord Eyez.
Unajua maisha yana milima na mabonde ndio nimekuwa mtoto wa kiume naweza kuvumilia lakini ni wakati mgumu sana kwangu na vitu ambavyo sijazoea, nimepitia maisha ambayo sijawahi kuyaona mengine,lakini all in all King Eazy kuna trak mpya inakuja so keep tuning, media support nini cause am not a criminal.”



     Kwa upande wake mwanasheria wake ambaye alisema lengo la kukutana na waandishi wa habari ni kuweka ‘record’ sawa tofauti na watu walivyolisikia tuki hilo, alidai kuwa tarehe 20 mwezi uliopita Lord Eyez alipigwa simu na mtu ambaye walikuwa wamefahamiana kwa muda mfupi na kuamini kuwa alimtaka kwenda kuzungumza masuala ya kijamii.

Friday, November 9, 2012

0

LORD EYEZ KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI HAPO KESHO

Posted in , ,
 


Rapper wa kundi la Nako 2 Nako Soldiers na Weusi, Lord Eyez, kesho anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari kuelezea shutuma dhidi yake za kudaiwa kushiriki kuiba vifaa vya gari vya Ommy Dimpoz.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rapper wa Arusha ambaye pia ni member wa Weusi, Nikki wa Pili, Lord Eyez atakuwa na mwanasheria wake.
Amesema mkutano huo na waandishi wa habari utafanyika katika hoteli iliyopo jirani na Mlimani City, jijini Dar es Salaam.
Lord Eyez yuko nje kwa dhamana na anakabiliwa na makosa zaidi ya 30 katika kesi hiyo.

Monday, September 10, 2012

0

Ommy Dimpoz - Baadae (Official Video HD). #My Video Of The Year Kwa Sasa

Posted in


 HII VIDEO NI NEXT LEVEL, WATANZANIA TUNAPIGA HATUA KATIKA TASNIA YA KIMZIKI
Artist: Ommy Dimpoz
Song: Baadae
Prod: Man Walter / Combination Sound
Direc: Adam Juma / Visual Lab

Thursday, July 12, 2012

0

Ningependa Arusha Wawe Na Joint Nzuri Kama KIGOMA ALL-STARS, NYEUSI haitoshi.

Posted in , , , , ,
Ningependa Arusha Wawe Na Joint Nzuri Kama KIGOMA ALL-STARS, NYEUSI haitoshi.

Huu ni mwaka ambao mkoa wa Kigoma utaongelewa sana kwenye burudani. Hongera nyingi ziende kwa yule aliyekuja na wazo hili lenye thamani ambalo limeunyanyua mkoa wa Kigoma katika kipindi kifupi mno.
Tangu itoke Leka Dutigite, Kigoma imejipatia sifa kubwa kwa kujulikana miongoni mwa wasanii waliojuu kwenye muziki wa kizazi kipya nchini kuwa wanatokea huko.
Ukizungumzia Diamond Platnumz na ukaona jinsi kijana alivyofanikiwa mpaka kupiga show Big Brother, ni halali uheshimu mkoa ulio asili yake, Kigoma. Tunafahamu kimaendeleo Kigoma ni miongoni mwa mikoa iliyonyuma kwa Tanzania. Wanapaita ‘Kigoma mwisho wa reli’. Jitihada hizi za mbunge wa Kigoma kaskazini, Mheshima Zitto Kabwe kuwapa support wasanii wenye asili ya Kigoma, sasa zimegeuka mfano wa kuigwa. 
Tangu wimbo ‘Leka Dutigite’, neno la kiha lenye maana ya Acha Tujidai, Kigoma umekuwa ni mkoa unaojadiliwa sana na wapenzi wa burudani mitaani na kwenye mitandao ya kijamii. Na hapo ndo utakapogundua kuwa Tanzania hakuna ukabila. Watu wa mikoa mingine wameupenda wimbo huu na kuwapongeza wasanii hao.
Ni wimbo uliofanywa na masupastaa haswaa wa Tanzania. Diamond, Peter Msechu,Ommy Dimpoz, Baba Levo, Banana Zorro, Chege, Mwasiti, Linex, Queen Darling, Rachel na wengine wasanii waliojuu sana nchini. Ni movement ambayo ikiwa nyuma ya mbunge mwenye kipaji cha uongozi, Mhe. Zitto, inayoweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye mkoa huo, kiuchumi na kisiasa.
Ni muungano unaoweza kupeleka maendeleo makubwa kwa kutumia mwavuli wa burudani. Ni movement ambayo itawaamsha wasanii wengine na hata watu wa kawaida kuthamini asili yao. Wanasema mtu asiyekuwa na kwao ni sawa na mtumwa. Itawaamsha wasanii waliopo Dar es Salaamn(kitovu cha tasnia ya burudani nchini) kujivunia mkoa ama hata kijiji anachotokea. Chema vizuri kuigwa.
Mikoa mingine haitakuwa na hasara ikifanya hivyo pia. Uzuri wa muungano kama huu, huchangia kukua kwa sanaa kwenye mkoa husika. Tangu Leka Dutigite itoke, kuna wasanii wengi wachanga wa mkoani Kigoma waliopata morali ya kuongeza juhudi zaidi kimuziki ili wafanikiwe na hatimaye kupewa heshima kama hiyo ya kujiunga na wakali wa mkoa huo. Japo baadhi yao kama wanavyosema kuwa Kigoma ni asili yao tu lakini hawakukulia huko, asili ipo pale pale na ni jambo la msingi kuutangaza.
Baada ya kitendo hicho, leo hii watu wengi wametamani wasanii wa mikoa yao wafanye kitu kama hicho pia. Huo ni wivu wa maendeleo kama asemavyo Monty Khatau Ezel, “Nimevutiwa na hiyo kitu, natamani ningekuwa natokea Kigoma,nina ugonjwa wa wivu wa maendeleo,najivunia kutokea kusini,LINDI wajiandae mafanikio yanawajia.”
Ibrahim Athumani Masokola naye anasema, “Nahisi katika mambo ya kuiga kwa baadhi ya watu kama waheshimiwa ni pamoja na hili analofanya mhe Zitto kwani ni njia mojawapo ya kuwafikia wananchi kwa urahisi HONGERENI SANA WOTE mlohusika kwa namna moja au nyingine.”
Naye Zulu Agrey Mnkeni anasema, “Natamani nami ningekuwa wa KIGOMA ila ndo bahati mbaya natoka KILIMANJARO naogopa kuitwa MKABILA.”
Kitendo hicho cha Mheshimiwa Zitto kuungana na wasanii ili kuutangaza mkoa wa Kigoma,kinamweka karibu zaidi na vijana waliowengi nchini na kumsafishia njia yake kwa mambo makubwa zaidi katika career yake kama mwanasiasa. Hongereni Kigoma All Stars!
Photos by: Bongo5.com

Thursday, May 24, 2012

0

Dimpoz ana SHEPU ya KIKE - Cyrill

Posted in ,


Siku chache baada ya msanii Cyrill kukataliwa kugonga show pale maisha club na Baraza la sanaa (Basata) kwa maelezo kuwa si mtanzania mpaka pale alipotoa vithibitisho, mengine yameibuka.
Hili limeibuka baada ya mkali wa 'nai nai' Ommy Dimpoz kuongea kwenye mahojiano na kituo kimoja cha Radio akimkandia live Cyrill kuwa msanii huyo hafanyi show kabisaaa.
Kwa upande wake Cyrill nae ktk mahojiano na Radio moja jijini Dsm amejibu mapigo hayo na kwenda mbali zaidi na kudai kuwa Ommy Dimpoz ana tabia za kike za kuzungumza zungumza hovyo na kumtaka siku nyingine akiwa na interview ajipange sio kuropoka hovyo mambo yasiyomhusu.
" Jamaa anaonyesha ni jinsi gani amechezea madarasa machache sana tena kwa muda mrefu, tena kuna siku nilimtizama nikamuona ana shape ya kike!!!!!!
Sasa unaambiwa yote haya yametokana na kuzuiliwa kwa Cyrill kuzuiliwa kugonga ile show na BASATA last week, huku Dimpoz akidai kuwa Cyrill anamtangazia kwa watu kuwa yeye ndiye aliyepeleka taarifa Basata kuwa jamaa sio mbongo ili azuiliwe kugonga show siku hiyo ambapo Dimpoz naye alikuwa na show yake pande za Bilicanas.

Friday, May 4, 2012

0

Ommy Dimpoz Aachia Ngoma Mpya (Download Hapa)

Posted in
Baada ya kufanya vizuri ile mbaya na track yake 'NAI NAI'  aliyoaichia mwaka jana na kufanikiwa kulamba tuzo 2 za Kili MUsic Awards hivi majuzi, Ommy Dimpoz  au unaweza kumwita Super Handsome kama anavyopenda kujiita yeye mwenyewe, amedondosha kazi mpya.

Kama vile kutaka kuonyesha kazi yake ya kwanza ya 'NAI NAI' hakubahatisha, leo hii amekuja na kitu kinaitwa 'BAADAE'.

Haya kazi kwako sasa kusikiliza na kujua kama ile ya kwanza 'NAI NAI' alibahatisha au hata hii ITABAMBAAA!
Download Buree hapa.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ