WALICHOKIONGEA WEUSI JUU YA VIDEO YAO ‘NJE YA BOX’ KUCHEZWA CHANNEL O.
Posted in WEUSI
Jana ilikuwa siku nzuri kwenye historia ya muziki ya kundi la Weusi linaloundwa na wasanii watano kutoka Kaskazini mwa Tanzania, Arusha, baada ya video ya wimbo wao ‘Nje ya Box’ kuchezwa Channel O.
Joh Makini aka Mwamba wa Kaskazini anaamini walichelewa tu kufika hapo walipofika, lakini pia akawashukuru wale wote waliofanikisha wao kufika pale walipofika.
Ameeleza pia sababu zilizomfanya achelewe kufika hapo na kudai kuwa kutokuwepo umoja kati ya wasanii wa Tanzania kuzisukuma kazi zao ni moja ya kikwazo, na kuutolea mfano umoja uliopo kati ya wasanii wa Nigeria ambao umewawezesha kuiteka Afrika na kuvuka mipaka.

















