ALLY KIBA KUFANYA SHOW YA KIHISTORIA YA MWAKA
Posted in Ally KibaNDANI ya wiki moja ijayo, Sikukuu ya Idd Mosi itaadhimishwa ambapo sambamba na hilo, mkali wa wakali kwenye Bongo Fleva, Ali Kiba anatarajia kuiandika historia kubwa ya mwaka katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar.
Mkali huyo anayetamba na nyimbo kali kama Dushelele, Single Boy, Nakshi Nakshi, Mac Muga, Cinderella na Karim amesema ataitumia shoo hiyo kuweka heshima yake kwa levo za kimataifa hivyo mashabiki watarajie maajabu.
“Ni shoo ambayo nitaandika historia ya mwaka, mara ya mwisho Dar Live nilifanya shoo mwaka jana lakini mwaka huu itakuwa balaa zaidi,” alisema Kiba.
Mratibu wa Dar Live, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ amesema siku hiyo itakuwa ni shangwe mwanzo mwisho kwani asubuhi kutakuwa na shoo maalum ya watoto kabla Kiba, Wanaume Family (Chegge, Temba, Aslay na Bi. Cheka), Bendi ya Mapacha Watatu na H. Baba hawajalivamia jukwaa kuanzia nyakati za jioni.















