Next
Previous
Showing posts with label Lady Jay Dee. Show all posts

Sunday, February 2, 2014

0

HIZI NI BAADHI YA NYIMBO ZILIZOTOKA TAREHE 31.JAN NA 1 FEB. || PAKUA NA SIKILIZA HAPA

Posted in , ,



Friday, December 20, 2013

0

KAMA HUWEZI YA RAMA DEE NA JAY DEE KUFANYIWA VIDEO NDANI YA NCHI TATU

Posted in ,

Msanii mkongwe wa r&b Bongo, Rama Dee ambaye anamiliki tuzo ya wimbo bora wa RnB aliyoichukua kupitia wimbo wake wa ‘Kuwa na subira’, ambaye kwa sasa maskani yake yapo sana Australi ambapo anaisi na mkewe wakiwa na mtoto mmoja amefunguka juu ya mpango wake wa kushuti video ya ‘Kama huwezi’.

http://baabkubwamagazine.com/wp-content/uploads/2013/12/Rama-dee1.jpg‘Kama huwezi’ ni wimbo aliomshirikisha mwanadada Lady Jay Dee ambao umekuwa gumzo sana kiasi cha watu wengi kuhitaji kuona kwenye video ile chemist iliyotumika kuitengeneza ngoma hiyo kiasi cha watu wengine kutengeneza slide show yenye wimbo huo na kuitupia youtube huku ikikamata viewers kibao. Akizungumza kwa njia ya simu ndani ya Power Jams ya East Africa Radio alifunguka juu ya sababu inayoichelewesha video hiyo.
“Nia yangu ipo palepale kwamba ‘Kama Huwezi’ itahusisha nchi tatu kama location ya video hiyo. Nchi hizo ni hapa Australia, South Africa ambapo ndege nitakayopanda kuja nayo Dar itapita na kukaa muda mrefu kabla ya kuja huko na mwisho ni Tanzania jijini Dar es salaam ambapo ndipo hata shot zote za Jide zitapigwa hapo.” – Rama Dee.

Sunday, August 18, 2013

0

LADY JAY DEE - YAHAYA (OFFICIAL VIDEO)

Posted in

Thursday, August 15, 2013

0

LADY JAY DEE KUFANYA TRACK NA NGULI WA MUZIKI AFRIKA "SALIF KEITA"

Posted in ,


Leo nimekaa na Salif Keita, Tuka shake hands, tuka hug, tukapiga mapicha mbali na yote kuna kitu kikubwa kinakuja kati yangu na yeke.... Sijapendezwa na alieondoka na bag langu la camera amesababisha nimeshindwa ku post picha..

Thursday, July 25, 2013

0

MACHOZI BAND NA PROF. JAY KUJA ARUSHA (eid mosi na eid pili) | ARUSHA TOUR-TeamAnaconda

Posted in ,

Monday, July 15, 2013

0

DUDE AUVAA uYAHAYA KATIKA VIDEO MPYA YA LADY JAY DEE

Posted in , ,


Video ya hitsong ya mwanadada komando Lady Jay Dee imeanza kushutiwa leo jioni, na DUDE ndiye aliyevaa uhalisia kama YAHAYA kwenye video hiyo. KAA TAYARI kuiona video hiyo

Wednesday, July 3, 2013

0

GOOD MUSIC: RAMA DEE FT. LADY JAY DEE - KAMA HUWEZI

Posted in ,

Sunday, June 30, 2013

0

RAMA DEE FT. LADY JAY DEE : TAARIFA JUU YA TRACK YAO

Posted in ,
RAMA DEE anataraji kutoa ngoma yake nyingine … Mshindi huyo wa tuzo za Kili, yaani KTMA2013 kwenye muziki atafanya hivyo hivi karibuni ambapo ndani ya ngoma hiyo ameshirikisha mwanadada LADY JAYDEE
Ngoma hiyo bado haijafahamika jina, but we’ll tell you as soon as tukiipata …

Monday, June 24, 2013

0

HUU NDO UKWELI KUHUSU WIMBO YAHAYA WA LADY JAY DEE

Posted in ,

YAHYA: A New TAPELI In ARUSHA

Katika kusikiliza wimbo mpya ya mwanadada LADY JAYDEE uliotoka hivi karibuni ukitambulika kwa jina YAHYA, nikaona kama ina ukweli fulani ndani yake na ndipo nilipoamua kumuuliza muhusika na kunijibu kuwa Yahya ni wimbo alioutunga kutokana na tabia za baadhi ya watu tunaoishi nao katika maisha yetu ya kila siku na maisha yao ni uongo wa kusabisha utapeli kwa watu na mali zao akiwemo huyo YAHYA.

Katika pitapita na uchunguzi, GongaMx TEAM imegundua kuwa YAHYA yupo na anaendelea na mambo yake ya utapeli na uongo baada ya kufuma taarifa kwenye mtandao wa jamii wa Facebook iliyoandikwa na Mr. JOHN wa huko Arusha kuwa YAHYA aka HISBERT akimtambulisha kama “A New TAPELI IN ARUSHA” kuwa amefanikiwa kukutana na YAHYA na ameweza kuhadithia aliyokutana nayo baada ya kukutana nae.

JOHN: I met this guy last night in the Heineken UEFA final @ Mango Tree,,, He just came and show up to us and introducing himself as a Immigration Officer from dar es salaam and he is in Arusha for special Task, especially for us MUZUNGU who lives here since most of us are illegal here. He told us not to tell anyone that we met him and he wanted to meet us next day >TODAY> for lunch because he had our files and we were the target by Immigration of Tanzania.

Sunday, June 23, 2013

0

ONA JINSI MWANA-FA ALIVYOLAZIMISHWA KUTAJA JINA LA "JAY DEE" KATIKA SHOO

Posted in ,
Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Jay Dee.
Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.
Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.
"  Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.   "

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.

Saturday, June 15, 2013

0

VIDEO: SHOW YA MIAKA 13 YA LADY JAY DEE KATIKA MUZIKI

Posted in

Friday, June 14, 2013

0

EXCLUSIVE PHOTOS TOKA NYUMBANI LOUNGE: LADY JAY DEE'S ANNIVERSARY

Posted in
 Lady Jay Dee Akiperform
Watu walivyojaa
Prof J. Backstage

Mh. Sugu Alivyowasili

0

LADY JAY DEE - YAHAYA (LYRICS)

Posted in


Chorus:
Yahaya unaishi wapi
Kwani jina lako halisi nani Yahaya eeehh
Oooh Yahaya, Oooh Yahaya, Oooh Yahaya
Maskani yako Kinondoni
Nyumba namba haijulikani Yahaya eeeehh
Oooh Yahaya, Oooh Yahaya

VERSE 1:
Huyu kijana mwenzetu, Kila siku tupo nae maskani
Anakula ofa za watu, Anapoishi hata hapajulikani
Tumetafuta, tumeuliza, hakuna ajuae
Anavyozuga, anavyopita
Si umdhaniae
Na hafananii kabisa, na fix anazofanya
Akidanganya kwa kina
Unaingia kingi unafuata, kumbe hana helaaaa
Longo longo nyingi

Rudia Chorus:

VERSE 2
Kwa story za vilingeni, Utafikiri kweli yeye ndio boss
Suruali zake na mashati, Anasema anafanya kazi bank
Mara anasema usalama wa Taifa, Hakuna ajuae
Kalubandika wa kizazi kipya, usomdhaniae
Na hafanii kabisa, na fix anazofanya
Akidanganya kwa kina
Unaingia kingi unafuata, kumbe hana helaaaa

Ooooh Yahaya

Sunday, June 2, 2013

0

MISS JUNE: LADY JAY DEE NA RATIBA YAKE PANA MWEZI HUU

Posted in ,

Saturday, May 25, 2013

0

LADY JAY DEE AMSHANGAA MWANA FA KWA ALICHOKIFANYA: SOMA ALIICHOKISEMA

Posted in , ,
Kutokana na JIDE kuwa na show yake kubwa mnamo tarehe 31 mwezi huu pale nyumbani lounge ,Sasa rafikiye wa karibu sana MwanaFA inaonyesha naye ameanda show yake siku hiyohiyo  ya Tarehe 31,Zaidi ya yote mwana FA akawachukua  wasanii walio jitoa katika show ya JIDE kama Linnah  sa kutokana na sitofahamu hiyo mtandao huu wa thechoicetz uliweza kumtafuta JIDE kupitia twitter na kumuu liza juu ya hili swala naye aliweza kutoa yake anayo yafikiria,pia mtandao huu wa thechoicetz ulimtafuta  MwanaFA lakini mwanaFA hakuweza kutujibu swali tulilo muuliza hadi muda huu


Hivi ndivyo jide ALIVYO TUJIBU

Wednesday, May 15, 2013

0

HII NI SERIES MPYA KATIKA SAKATA LA LADY JAY DEE: WARAKA TOKA KWA WADAU

Posted in

Wadau wa huu muziki wameniomba pasipo ku-edit huu waraka wa kwanza kati ya 88 uende hewani. Ni waraka unazungumzia hali ya muziki na vita ya wasanii na wale wanaoitwa wanyonyaji wa muziki. Blog iko kwa kila upande, hivyo nauwakilisha kwenu waraka ambao mdau wake wameomba asitajwe kwa sasa..

WARAKA NAMBA 1(ZIPO 88) KILA WIKI UTAPATA WARAKA MMOJA-

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa pili ulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.
Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?

Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?
Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.
Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge na Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)
Naanza kupatwa na wasiwasi nikijiuliza, endapo Lady JD angekuwa amegombana na msanii mwenzake mkubwa kama Prof Jay, Ray C au Juma Nature wanasiasa wangeingilia kati? Ni wazi wasingesogea kwa kuwa hakuna maslahi zaidi ya kuingilia mgogoro huu ambao hawataki jamii ijue maovu yao.

0

BARNABA NA LINAH HATIMAYE KUFANYA SHOW YA LADY JAY DEE | ANGALIA VIDEO WAKILIONGELEA

Posted in , ,
Zikiwa zimebaki wiki kadhaa kufikia show ya mwanadada LADY JAYDEE kufanyika, mwanamuziki BARNABA na LINAH [THT] wameongelea ushiriki wao katika MIAKA 13 ya mwanadada huyo ...
Hivi karibuni kulikuwa na minong'ono kuwa huenda kuna baadhi ya wasanii kutoka THT ambao nao walikuwa kwenye orodha ya wasanii watakaotumbuiza siku hiyo huenda wasitokee siku ya show hiyo ...
Wasanii hao ambao walitajwa kuwa ni BARNABA pamoja na LINAH walikuwa wakihisiwa kutokutokea siku ya show hiyo sababu huenda wanaweza kuwa wamezuiwa na kiongozi wa Tanzania House Of Talent (THT) ...

Tuesday, May 14, 2013

0

LADY JAY DEE KUKIMBILIA NCHI JIRANI

Posted in

Ni masaa machache tu yaliyopita mwanamuziki LADY JAYDEE ameandika kutaka kihama nchi yake hii na kuelekea nchi jirani ya Jamhuri ya watu wa KENYA ...
Jide anafikiria kwenda kuomba uraia huko ama MALAWI katika kuonekana kutaka kujinasua kutoka katika jambo fulani ...
Mwanamuziki huyo ame-tweet kupitia mtanadao wa kijamii wa twitter na kuandika @JideJaydee "Kuna muda pesa tu ndio inaongea sijui nihamie Kenya nikaombe uraia huko? Au Malawi labda, mtanifuata?...
Ni nani atamfuata?? Je ni kuhusu ugomvi wake ulioibuka hivi karibuni ??
Keep it right here while we trying to know ...

Friday, May 10, 2013

0

LADY JAY DEE AFUNGULIWA KESI MAHAKAMI

Posted in


Hii Kali !!!

Kupitia moja ya kurasa za kijamii ya mwanamuziki Lady JayDee ameandika kuwa amepata taarifa kuwa amefunguliwa kesi mahakamani ila hajasema ni nani aliemfungulia kesi hiyo na ni mashtaka yanayohusu nini ...


Bado tunafuatilia kwa karibu kujua ni ni hasa kimemkuta mwanadada huyu ..

Wednesday, May 8, 2013

0

ZITTO NAYE ALIONGELEA SUALA LA LADY JAY DEE NA CLOUDS MEDIA

Posted in , ,
Mgogoro kati ya Lady JayDee a.k.a Anaconda na uongozi wa Clouds Media Group bado ni issue, mengi yameshazungumzwa lakini kuna tweet moja ambayo mh. Zitto Kabwe ameona inafaa zaidi kuleta mabadiliko katika mzozo huo.

Zitto aliirudia Tweet ya Absalom Kibanda ya May 5 iliyosemeka.
 “An Iron Lady! Turn back and forgive. There’s power behind forgiveness”
Lady JayDee nae akamjibu:
@absakibanda Nakuelewa sana brother
Tweet ya Absalom ilimvutia zaidi Zitto Kabwe ambae aliandika:
“This tweet will surely bring peace. Watch “@absakibanda: @JideJaydee An Iron Lady! Turn back and forgive. There's power behind forgiveness”
Na akasisitiza zaidi na kusema hili ni neno la Busara:
“+1 in these words of deep wisdom “@absakibanda: @JideJaydee An Iron Lady! Turn back and forgive. There's power behind forgiveness”
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ