Muziki wa bogno umepiga hatua kubwa sana hasa katika mwaka huu. Mengi Yametokea, Vipaji vingi vimejitokeza. Mitindo mingi ya Kimziki na Dansi iliongezeka.
1. Kupaa Kwa Ommy Dimpoz
Pooooz kwa Poz...
 |
| Ommy Dimpoz Na Vanessa Mdee |
Huu ulikua ni mwaka wa kijana huyu ambaye alianza kwa kutoka na Nyimbo NAI NAI iliyompa tuzo za kili kwa kumshirikisha Ally Kiba, Akaja na BAADAE, na baadae akafunga mwaka kwa nyimbo ya ME & YOU ft. Vanessa Mdee. Kijana huyu ameepata mafanikio mengi na kupiga hatua moja ikiwa ni kufanya video nchini Afrika Kusini. Kijana huyu pia alitoa malalamiko ya kumshutumu Lord Eyez kuiba PowerWindow za Gari Lake(Rav4).
2. Kuendelea Kuvuma kwa WEUSI.
WEUSI ni Kundi Muanganiko wa wasanii wa Arusha toka kundi la N2N na RiverCamp likijumuisha Wasanii kama Lord Eyez, Joh Makini, G-Nako, Nikki Wa pili na Bonta. Kundi hili limekua na mafanikio mengi huku kashfa aliyoipata Lord Eyez, kulifanya lipate sifa mbaya na wale walioamini hilo.
3. Udhamini wa OSTAZ JUMA NAMUSOMA kwa WATANASHATI

Watanashati wamevuma sana katika mwaka huu, Wamemrudisha PnC katika Fani, Wameokoa kipaji cha Dogo Janja, Suma Mnazaleti kwa udhamini mzuri walionao. Kundi hilo lilizidi kuwa kubwa kadri mda ulivyokwenda, na wamevuma zaidi kwa nyimbo zao. Uwepo wa Marehemu Sharo Millionea na Teja Kitale uliweka uamsho katika kundi.
HONGERA OSTAZ JUMA