Next
Previous
Showing posts with label Simba SC. Show all posts

Monday, September 30, 2013

0

WAZUNGU WAWEZE WANA NINI?? NA SISI TUSHINDWE KWA NINI?? | KIBADENI ALIONGELEA HILO

Posted in ,
KOCHA mkuu wa klabu ya Simba, Abdallah Kibaden inaelekea amejiuliza “makocha wazungu wanaweza wana nini, na makocha wazawa wanashindwa wana nini?”

Msimu uliopita, akiwa kocha mkuu wa klabu ya Kagera Sugar ya Bukoba alihakikisha inazichapa klabu za Simba ya Yanga ambazo zilikuwa zinanolewa na makocha wazungu katika Ligi Kuu ya Bara.

Msimu huu, Kibaden aliitosa Kagera Sugar akaingia mkataba na Simba. Klabu hiyo na nyingine inazoshiriki Ligi Kuu zinafanya vizuri tofauti na zile zinazofundishwa na wageni au makocha wa Kizungu.

Simba ndiyo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 14, ikifuatiwa na JKT Ruvu iliyo chini ya mzawa Mbwana Makata yenye pointi tisa.

Hadi mzunguko wa tano Jumapili iliyopita, timu zinazonolewa na makocha wageni zinaonekana kuchechemea. Azam FC iliyo chini ya Mwingereza, Stewart Hall ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi tisa huku Kagera Sugar inayonolewa na Mganda Jackson Mayanja ikiwa nafasi ya sita na pointi nane.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga chini ya Ernie Brandts raia wa Uholanzi, ipo nafasi ya nane ikiwa na pointi sita. Timu zote hizo zimecheza michezo mitano.

Kwa muda mrefu Simba ilikuwa chini ya makocha wa kigeni hasa wazungu kutoka nchi mbalimbali za Ulaya, wa mwisho wa kigeni alikuwa raia wa Ufaransa, Patrick Liewig.

Simba haikuwa katika kiwango chake chini ya kigeni hasa kuanzia miaka hii ya 2000, na hata mwaka huu ilipoachana na Liewig haikuwa katika kiwango cha kuridhisha.

Ukimwacha Patrick Phiri wa Zambia aliyewahi kuipa ubingwa klabu hiyo yenye maskani yake Mtaa wa Msimbazi, Dar es Salaam, makocha wengine kama Neider dos Santos (Brazil), Nielsen Elias (Brazil), Krasmir Benzinski (Bulgaria), Milovan Cirkovic na Liewig hawakuwa na matokeo ya uhakika japokuwa timu ilikuwa ikipata ushindi na hata ubingwa.

Hata makocha wageni waliofanikiwa katika kikosi hicho, mara nyingi wasaidizi wao walikuwa wazawa kama Amri Said, Kibadeni na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’. Kazi kubwa ya wazawa ni kuwa kiunganishi kati ya kocha na wachezaji.

Kitu kinachoitafuna Simba inayoundwa na wachezaji wengi chipukizi, ni saikolojia. Vijana wengi wanaonekana kucheza vizuri, lakini bado hawajiamini wawapo uwanjani.

Hilo huwa jukumu la kocha na benchi zima la ufundi (wasaidizi hasa), lakini kwa vile benchi la ufundi linadhibitiwa na wazawa Kibadeni na Julio, inawawia rahisi kuzungumza nao kwa Kiswahili kuwaweka sawa vijana hao ambao sasa wanafanya vizuri. Ukiwachanganya na wazoefu kama Hamisi Tambwe, Henry Joseph na Amri Kiemba, Simba sasa ipo moto.

Inapotokea kocha wa kigeni akawa na jukumu moja tu la kufundisha timu na kurudi hotelini, huku akiwa hana muda wa kutazama hali za kisaikolojia za wachezaji wake huku akishindwa kujua matatizo ya wapiganaji wake, mambo huwa tofauti uwanjani.

Itazame Yanga sasa, inaonekana moto uwanjani kutokana na kuwa na wachezaji wengi wazoefu huku uwepo wa kocha msaidizi Fred Minziro ukisaidia kuwaweka sawa kisaikolojia wachezaji wote.

Katika miaka ya 2000, Yanga imewahi kufundishwa na Jack Chamangwana (Malawi), Milutin Sredojevic ‘Micho’, Dusan Kondic, Kosta Papic (wote Serbia), Sam Timbe (Uganda), Tom Saintfiet (Ubelgiji) na Brandts raia wa Uholanzi ambaye hadi sasa anainoa timu hiyo.

Mara nyingi makocha wote hao wamepata mafanikio kutokana na usaidizi wa karibu na makocha wazawa. Na mbaya zaidi makocha hao wazawa wengi wao wana elimu ama zinazolingana au zinazokaribiana na zile za makocha wa kigeni.

Tatizo linaloikabiri Simba inapokuwa na makocha wa kigeni ni lile lile lililopo kwa makocha wa Yanga. Tena mbaya zaidi kwa timu hizi, ni kuwa na lundo la wachezaji ambao lugha ya Kiingereza inakuwa tatizo kwao.

Ukichanganya kocha wa kigeni kutokuwa na mazoea ya kutazama hali ya kisaikolojia kwa wachezaji ambao hawana msingi wa kufundishwa, halafu tatizo la lugha likihusika hapo timu lazima itayumba hata kama inakuwa na mwalimu mwenye ujuzi mwingi.

Makocha hawa wa kigeni hasa wasiofahamu lugha ya Kiswahili, hupenda kuwatumia wazawa kama wakalimani, hapo ndipo tatizo linapotokea. Katika hali ya kawaida, tafsiri inaweza kuwa tatizo, kile anachomaanisha kocha si kinachowafikia wachezaji.

Tazama Azam ikiwa chini ya Hall, bila ya ushindi wa mechi ya wikiendi iliyopita dhidi ya Yanga, mambo yangekuwa tofauti. Ana kikosi kilichosheheni wachezaji kutoka sehemu kubwa ya Afrika lakini mambo bado ni magumu.

Kuwa na wachezaji bora kunasaidia kutengeneza timu bora. Azam yenye wachezaji bora ama wachezaji hawauelewi mfumo au haukubaliki. Pia mambo mengine nje ya uwanja yanachangia hasa kutokana na tabia ya misimamo ya kocha.

Aidha, kuna matatizo katika mfumo wetu wa soka. Kuna wakati mchezaji anafika Yanga au Simba bado anafundishwa namna ya kukokota mpira. Kwa nini? Sababu ni kwamba walisajiliwa si kwa ubora bali ‘kufanikiwa’ kuzifunga Simba na Yanga na ghafla anateuliwa Taifa Stars.

Saturday, July 13, 2013

0

SIMBA YAMSAJILI MFUNGAJI BORA WA KAGAME CUP 2013

Posted in , ,
.
Simba sports Club ya Dar es Salaam imefanikiwa kumsajili mfungaji bora wa michuano ya Kagame Cup 2013 Hamis Tambwe kutokea Vital O ya Burundi kwa kumpa mkataba wa miaka miwili July 12 2013 kuanza kuwatumikia wekundu hao wa Msimbazi kwa mujibu wa shaffihdauda.com
.

Thursday, May 16, 2013

0

KOCHA MKUU TAIFA STARS ATAJA KIKOSI CHA KUIVAA MOROCCO | TIKETI ZA MECHI YA SIMBA NA YANGA ZAANZA UZWA

Posted in , , ,
Na Soka In Bongo
TAIFA_STARS-FRAMED>> TANZANIA YAJITOA MICHUANO YA COSAFA
>> TIKETI SIMBA, YANGA KUANZA KUUZWA KESHO
>>TIKETI NI KUANZIA SH. 5,000 HADI 30,000
PATA HABARI KAMILI:






Release No. 084
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 16, 2013
KIM ATAJA 26 STARS WA KUIVAA MOROCCO
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 16 mwaka huu) ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.
Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku akiacha wengine watatu aliokuwa nao kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Morocco ambapo Taifa Stars ilishinda mabao 3-1.
Wapya aliowaita katika kikosi hicho kitakachoingia kambini Mei 20 mwaka huu, saa 1 jioni kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam ni Ally Mustafa, Vicent Barnabas, Juma Luzio, Haruna Chanongo, Mudhathiri Yahya na Zahoro Pazi. Wachezaji aliowaacha ni Shabani Nditi, Nassoro Masoud Cholo na Issa Rashid.
Kikosi kamili cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kabla ya kwenda Morocco kitapita jijini Addis Ababa, Ethiopia kucheza mechi ya kirafiki Juni 2 mwaka huu dhidi ya Sudan ni kama ifuatavyo;
Makipa ni nahodha Juma Kaseja (Simba), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar) na Waziri Salum (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mudathiri Yahya (Azam) na Salum Abubakar

Saturday, May 11, 2013

0

KLABU YA SIMBA NA MASHABIKI WAO WAJIPANGA KUTIBUA RAHA YA KUSHANGILIA UBINGWA KWA YANGA

Posted in ,

Mashabiki wa klabu ya Simba wamesema wanaimani na chipukizi wao kuwa watawafunga Yanga katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu Tanzania bara utakaofanyika tarehe 18 mwezi Mei. Mashabiki hao wamesema wanauhakika na ushindi dhidi ya Yanga, kwani nia yao ni kuondoa utamu wa kutwaa kombe la ligi kwa vile wanajua siku ya tarehe 18 baada ya mechi ndipo Yanga atakabidhiwa kombe hivyo kama Yanga atafungwa na Simba kwenye huo mchezo basi raha ya kushangilia itakuwa imeingia dosari, lakini mchezaji wa zamani wa Simba Zamoyoni Mogella amesema chipukizi hao wa Simba wataweza kufanya maajabu hayo kama wataweza kutumia vyema kipindi cha kwanza ili wajipatie magoli ya kutosha mapema bila kuchelewa hadi kipindi cha pili ambapo huwa wanachoka na kuwapa mwanya wapinzani wao. Simba inayoshikilia nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kwasasa imeamua kuwapa nafasi chipukizi wake kuonesha uwezo wao lakini vilevile kuwajenga ili waje kuchukua nafasi kwenye kikosi cha kwanza, chipukizi hao wamekuwa wakicheza mechi kadhaa za mwisho wa ligi na wanatarajiwa kushuka dimbani tarehe 18 dhidi ya Yanga. 

Wednesday, May 8, 2013

0

YANGA KUKABIDHIWA KOMBE KATIKA MECHI DHIDI YA SIMBA

Posted in , ,

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) litakabidhi kombe kwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga katika mechi yao ya mwisho ya ligi hiyo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Mei 18.

Akizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi ya TFF, Wallace Karia alisema kuwa wataikabidhi Yanga kombe hilo baada ya kumalizika kwa mechi hiyo ya kufunga msimu wa 2012/13 wa ligi.

Sunday, April 21, 2013

0

NA SOKA IN BONGO: VPL-YANGA 3 JKT RUVU 0, YANGA BADO POINTI 1 BINGWA!!

Posted in , ,
>>YANGA BADO COASTAL, SIMBA!!
>>LAKINI, AZAM AKIFUNGWA NA COASTAL JUMAMOSI IJAYO, YANGA BINGWA!!
Vinara wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Yanga leo wameipiga JKT Ruvi Bao 3-0 na kujiweka nafasi nzuri ya kutwaa Ubingwa kwa kuhitaji Pointi 1 tu kati ya Mechi 2 walizobakisha bila ya kujali matokeo yeyote ya Timu ya Pili Azam FC.
+++++++++++
MAGOLI:
Yanga 3
-Simon Msuva Dakika ya 45
-Hamis Kiiza 59
-Nizar Khalfan 65
JIK Ruvu 0
+++++++++++
Yanga sasa imefikisha pointi 56 wakifuatiwa na Azam FC wenye Pointi 47 na waliobakisha Mechi 3.
++++++++++++++++++++++++++++
MECHI WALIZOBAKISHA YANGA:
Mei 1: COASTAL v YANGA YANGA [MKWAKWANI]
Mei 18: YANGA v SIMBA [UWANJA wa TAIFA]

Tuesday, February 12, 2013

0

LIBOLO WAWASILI DAR KUKABILIANA NA SIMBA SC

Posted in ,
Timu ya mpira wa miguu kutoka Angola, LIBOLO FC yafika jijini Dar Es Salaam tayari kwa mchezo wao na Mabingwa Soka Tanzania Bara, Simba Sports Club.
Wapinzani hawa wa Simba wapo jijini kukipiga na timu hiyo katika kuwania Ubingwa wa Ligi Ya Mabingwa Afrika siku ya Jumamosi.
Libolo FC ilifika nchini siku ya Ijumaa ambapo ilifikia katika Hotel ya Double Tree ikiwa na wachezaji waliofika kama awamu ya kwanza ya timu nzima.

Saturday, October 27, 2012

0

YALIYOJIRI LIGI KUU TANZANIA BARA NA RATIBA YA MECHI ZIJAZO:: NA WENZETU SOKA IN BONGO

Posted in , , , ,

VPL: Simba yaipiga Azam, Yanga yaipiku Azam nafasi ya 2!!

Jumamosi, 27 Oktoba 2012 20:14
Chapisha Toleo la kuchapisha
VPL_LOGOKatika mfululizo wa Mechi za Ligi Kuu Vodacom, VPL, zilizochezwa leo, Mabingwa watetezi Simba wamefanikiwa kuichapa Azam bao 3-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuendelea kubaki kwenye uongozi huku Yanga, wakiwa huko Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha wakiifunga JKT Oljoro bao 1-0 na kuipokonya Azam nafasi ya Pili kwenye Msimamo wa Ligi.
++++++++++++++++++++++++++
MATOKEO/RATIBA:
Oktoba 27
Simba 3 Azam 1
JKT Oljoro 0 Yanga 1
African Lyon v Kagera Sugar
Mgambo JKT v Tanzania Prisons
Ruvu Shootings v Polisi Morogoro
++++++++++++++++++++++++++
Bao la ushindi la Yanga lilifungwa na Mbuyu Twite katika Dakika ya 53.
Katika Mechi ya Simba na Azam, John Bocco ndie alietangulia kuifungia Azam bao moja katika Dakika ya 5 lakini Simba ikazinduka na kupiga Bao 3 kupitia Felix Sunzu, Dakika ya 7, na bao mbili za Emmanuel Okwi.
++++++++++++++++++++++++++

Saturday, October 6, 2012

0

MPYA ZA LEO KUTOKA TFF, Na Wenzetu SOKA-IN-BONGO

Posted in , , , , , ,
>> YANGA, AFRICAN LYON KUTOVAA BEJI YA MDHAMINI!
>> WAAMUZI WATATU WAONDOLEWA, SIMBA YAPIGWA FAINI!
>> MECHI YA KAGERA SUGAR, YANGA YASOGEZWA!
>> LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 20!

LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 20
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana jana (Oktoba 5 mwaka huu) kupitia na kufanya uamuzi katika masuala mbalimbali na kupanga Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ianze kutimua vumbi Oktoba 20 mwaka huu.
TFF_LOGO12Timu zimepangwa katika makundi matatu ya timu nane nane ambapo zitacheza ligi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na ugenini. Mshindi wa kila kundi ndiye atakayepata tiketi ya kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao wakati timu ya mwisho kila kundi itashuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa.
Kundi A lina timu za Burkina Moro ya Morogoro, Kurugenzi Mufindi ya Iringa, Majimaji ya Songea, Mbeya City ya Mbeya, Mlale JKT ya Ruvuma, Mkamba Rangers ya Morogoro, Polisi Iringa na Small Kids ya Rukwa.
Ndanda FC ya Mtwara, Ashanti United, Green Warriors, Moro United, Polisi, Tessema, Transit Camp na Villa Squad zote za Dar es Salaam ndizo zinazounda kundi B wakati kundi C ni Kanembwa JKT ya Kigoma, Morani ya Manyara, Mwadui ya Shinyanga, Pamba ya Mwanza Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers ya Tabora.
Ada ya ushiriki wa ligi ni sh. 200,000 zinazotakiwa kulipwa kabla ya Oktoba 13 mwaka huu. Pia Oktoba 13 mwaka huu kutakuwa na kikao kati ya wenyeviti wa klabu zote zinazoshiriki ligi hiyo na Kamati ya Ligi ambapo pia itafanyika draw (ratiba).

Wednesday, October 3, 2012

0

MECHI YA WATANI WA JADI YAMALIZIKA KWA SULUHU.

Posted in , , , ,
Simba Na Yanga
Ni magoli ya Bahanuzi na Kiemba yaliyofanya mechi hii ya watani hawa irembwe kwa sare ya bao moja kwa moja. Amri Kiemba aliipatia timu yake ya Simba bao la kwanza katika dakika ya 5, huku Kijana toka Sengerema Saidi Bahanuzi akisawazisha bao hilo katika kipindi cha pili mnamo dakika ya 65, kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Simba kuunawa Mpira.
Katika mchezo huo mchezaji wa Yanga alizawadiwa Kadi nyekundu mnamo mwishoni mwa mechi, Huku Juma Kasseja akionesha umahiri wake kwa kuokoa Michomo mbalimbali.

Friday, July 27, 2012

0

Nani Kuibuka Kidedea??: Yanga VS Azam

Posted in , , ,
Ijumaa, 27 Julai 2012 11:59
Chapisha Toleo la kuchapisha
  • KAGAME_CUP_2012• NANI kulikwaa ‘BUTI la DHAHABU??’
Jumamosi Julai 28 Fainali ya Kagame Cup, Kombe la Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa Mechi kati ya Mabingwa watetezi Yanga na Azam FC.
Hakuna Mdau yeyote wa Soka mwenye uhakika kama Yanga watafanikiwa kutetea vyema Taji lao walilolitwaa Mwaka jana kwa kuwafunga Mahasimu wao Simba bao 1-0 kwenye Fainali au Timu mpya kwenye Mashindano haya, Azam, inaweza kujiwekea historia kwa kulibeba Kombe hili kwa mara ya kwanza.
Uhakika pekee uliokuwepo ni kuwa Kagame Cup inabaki tena Tanzania kwa mara ya pili mfululizo.
==========================
WAMEFIKAJE FAINALI:
YANGA
KUNDI C:
-Atletico 0-2
-El Salaam Wau 7-1
-APR 2-0
ROBO FAINALI:
-Mafunzo 1-1 [Penati 5-3]
NUSU FAINALI:
-APR 1-0 [Baada ya Dakika 120]
AZAM
KUNDI B:
-Mafunzo 1-1
-Tusker 0-0
ROBO FAINALI:
-Simba 3-1
NUSU FAINALI:
-Vita Club 2-1
==========================
YANGA-AZAM3NATIONAL_STADIUM2Hakika Fainali hii ni ngumu na imezua mjadala mkubwa hasa ikikumbukwa mara ya mwisho Timu hizi kukutana ilikuwa ni kwenye Ligi Kuu Vodacom Mechi ambayo Azam walishinda bao 3-1 lakini Mechi hii ilizua balaa kubwa baada kutokea vurugu kwa Mwamuzi Israel Nkongo mara baada ya kumpa Kadi Nyekundu Niyonzima wa Yanga na kusababisha Wachezaji kadhaa wa Yanga kupigwa Faini na kufungiwa kwa madai ya kumpiga Refa huyo.
==========================
WAGOMBEA ‘BUTI la DHAHABU’:
-Teddy Etekiama [Vita Club]=Bao 6
-Said Bahanuzi [Yanga]=5
-Hamisi Kiiza [Yanga]=5
-John Bocco [Azam]=5
-Suleiman Ndikumana [APR]=3
-Preus [APR]=2
-Abdallah Juma [Simba]=2
==========================
Mbali ya kuwa na Timu zilizosheheni Wachezaji mahiri Timu hizi pia zina Mastraika hatari mno ambao pia wana vita kubwa kati yao ya kuwania Tuzo ya Mfungaji Bora kwenye michuano hii ambayo hadi sasa alieshika Nambari Wani kwenye safu ya ufungaji ni Teddy Etekiam wa Vita Club mwenye Bao 6 na anafukuzwa na Wachezaji watatu wenye Bao 5 kila mmoja ambao ni Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza wa Yanga na John Bocco wa Azam.
Wachezaji wote hawa wana nafasi nzuri ya kuongeza Mabao wakati Timu zao zitakapocheza Fainali na ile Mechi ya kutafuta Mshindi wa Tatu.
RATIBA:
MSHINDI WA 3:
Julai 28 Jumamosi
[Saa 8 Mchana]
Vita v APR
FAINALI:
Julai 28 Jumamosi
[Saa 10 Mchana]
Azam v Yanga
KWA RATIBA na HABARI NYINGINE BOFYA: http://www.sokainbongo.com/kagame-cup-2012

Monday, May 28, 2012

0

Picha Za SIMBA SC Trophy Tour DarLIVE

Posted in , ,
KIPA wa Simba, Juma Kaseja jioni hii ameshindwa kujizuia lilipotajwa jina la Patrick Mafisango kwenye sherehe za ubingwa wa Ligi Kuu ya klabu hiyo na kujikuta akimwaga machozi kwenye ukumbi wa Dar Live, Mbagala, Dar es Salaam.
Kaseja alimwaga machozi wakati alipokuwa akipokea Medali kwa niaba ya marehemu Mafisango aliyefariki dunia wiki iliyopita kwa ajali ya gari maeneo ya Keko, Dar es Salaam ambapo alizikwa kwao DRC siku tatu baadae.
Kiungo wa Simba, Salum Machaku aliitoa Medali aliyokabidhiwa kwenye sherehe hizo kwa marehemu Mafisango ambapo Kaseja alinyamaza baada ya kubembelezwa na wachezaji wenzake na kuendelea na shughuli hiyo iliyofana na kuhudhuriwa na mamia ya wapenzi wa klabu hiyo.
.
Ukumbi pamoja na mapambo yaliyowekwa,  ulipendeza zaidi kwa mavazi ya mashabiki wa Simba ya rangi nyekundu na nyeupe ambapo Meneja wa Global Publishers Limited, Abdallah Mrisho alikabidhi Sh. Milioni 3 kwa Kaseja kama zawadi yao kwa Simba kutokana na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu.
Baada ya yote hayo, wachezaji na viongozi wa Simba walifungua shampeni na sherehe ikaanza rasmi, bendi ya Msongo Ngoma ikianza kutumbuiza, ikiongozwa na mwimbaji wake mkongwe, shabiki maarufu wa Simba, Mzee Muhiddin Mwalimu Gurumo.   (Stori imeandikwa na Bin Zubery wa Bongostaz.blogspot.com )
.
Amos Makalla Mbunge wa Jimbo la Mvomero,akimkabidhi medali Juma Kaseja nahodha wa Simba.
Kaseja akilia kumpoteza Mafisango.

Thursday, May 17, 2012

0

Mchezaji wa Simba Patrick Mutesa Mafisango afariki katika ajali ya gari

Posted in , ,
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, marehemu Patrick alipata ajali maeneno ya TAZARA alipokuwa akiendesha gari na kujaribu kumkwepa mwendesha pikipiki na kwa bahati mbaya gari lake likakosa uelekeo na kuingia mtaroni na kusababisha ajali iliyomwacha na majeraha makubwa ambapo aliaga dunia muda mfupi baadaye.
Patrick alijiunga kuichezea Simba SC akitokea timu ya Azam FC. Alizaliwa tarehe 9 Machi 1980 mjini Kinshasa, Kongo D.R.C lakini alikuwa raia wa Rwanda.
Amefariki siku chache tu baada ya kocha wa timu ta taifa ya Rwanda kumuita kujumuika katika timu ya Taifa ya nchi hiyo.
Poleni nyote mliofikwa na huzuni ya msiba huu!
Apumzike pema Patrick Mafisango.
ETERNAL REST GRANT HIM OH, Lord AND, LET PERPETUAL LIGHT SHINE UPON HIM.
AMEN.
0

KAGAME CUP: Klabu 12 kushiriki Dar, kugharimu Milioni 900!!

Posted in , ,


kagamecup07
Katibu Mkuu wa CECAFA, Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, Nicholas Musonye, amesema Timu 12 zitashiriki Mashindano ya Mwaka huu ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kagame Cup, ambayo yatagharimu Dola 600,000 (zaidi ya Shilingi Milioni 900) na yatachezwa Jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 23 hadi Julai 7.
Mwaka jana, michuano ya Kagame Cup, iliyodhamini wa na Kampuni ya Bia Tanzania TBL kupitia Bia yake ya Castle kwa Sh300 milioni, Ilifanyika Jjini Dar es Salaam na Yanga kuibuka Bingwa kwa kuichapa Simba kwa bao 1-0 kwa bao la dakika za majeruhi lililofungwa na Straika kutoka Ghana, Kenneth Asamoah.
Musonye alisema Ratiba ya michuano hiyo, ambayo itaonyeshwa moja kwa moja na Kituo cha TV cha Supersport, itapangwa baada ya Timu zote 12 kuthibitisha ushiriki wao.
Akifafanua kwa nini Tanzania inakuwa Mwenyeji wa Mashindano hayo kwa Miaka mitatu mfululizo, Musonye alisema ni sababu ya mafanikio yaliyopatikana katika mashindano ya Kombe la Chalenji na Kombe la Kagame Mwaka jana pamoja na uhakika wa udhamini.
Kawaida, zawadi za Washindi zimekuwa zikitolewa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambae ndie ametoa Kombe na pia hutoa Tuzo ya Dola 60,000 kwa Bingwa.
Mwaka jana timu 13 zilishiriki, ambazo ni Ulinzi (Kenya), Ports (Djibouti), St George (Ethiopia), El Merreikh (Sudan), Red Sea (Eritrea), Elman (Somalia), APR na Etincelles (zote toka Rwanda), Bunamwaya (Uganda), Vital'O (Burundi), Simba na Yanga za Tanzania
 
More News: www.sokainbongo.com

Monday, May 7, 2012

0

Photos Showing Celebrations of Winners in different Soccer Leagues

Posted in , , , ,
Juventus-Italy
Simba SC
FC PORTO
Celtic_Scotland
Borrusia Dortmund-Germany
Real Madrid CF


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ