Next
Previous
Showing posts with label Vodacom Premier League. Show all posts

Monday, July 22, 2013

0

LIGI KUU YA SOKA TANZANIA BARA 2013/2014 KUANZA AGOSTI 24

Posted in ,

20130722-084204.jpgLigi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa

2013/2014 inaanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa
viwanjani katika miji saba tofauti.

Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu
(Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu
bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.

Mechi za VPL za Agosti 14 mwaka huu zitakuwa kati ya Yanga na Ashanti
United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mtibwa Sugar na Azam (Uwanja wa
Manungu, Morogoro), na JKT Oljoro na Coastal Union (Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).

Wednesday, May 8, 2013

0

YANGA KUKABIDHIWA KOMBE KATIKA MECHI DHIDI YA SIMBA

Posted in , ,

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) litakabidhi kombe kwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga katika mechi yao ya mwisho ya ligi hiyo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Mei 18.

Akizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi ya TFF, Wallace Karia alisema kuwa wataikabidhi Yanga kombe hilo baada ya kumalizika kwa mechi hiyo ya kufunga msimu wa 2012/13 wa ligi.

Friday, November 9, 2012

0

KUTOKA TFF NA WENZETU SOKAinBONGO.com>> RATIBA YAREKEBISHWA KUPISHA MECHI YA STARS

Posted in , , ,
>> UCHAGUZI TAREFA, TAFCA SASA DESEMBA 22
>> TFF YATOA PONGEZI KWA UONGOZI MPYA FA MWANZA
TFF_LOGO12Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF, imefanya mabadiliko madogo ya ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom, VPL, ili kupitisha Mechi ya Kirafiki ya Kalenda ya FIFA kati ya Taifa Stars na Kenya, Harambe Stars, itakayochezwa Novemba 14 Jijini Mwanza na mabadiliko mengine yanahusu Ratiba ya Ligi Daraja la Kwanza, FDL.
Zifuatazo ni Taarifa kamili za TFF:
Release No. 180
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Novemba 9, 2012
MECHI TANO VPL ZAPISHA TAIFA STARS
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imefanya mabadiliko madogo ya ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom ili kupitisha mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kati ya Taifa Stars na Kenya (Harambe Stars) itakayochezwa Novemba 14 mwaka huu jijini Mwanza.
Mechi tano za ligi hiyo zilizokuwa zichezwe Novemba 11 mwaka huu, zimerejeshwa nyuma kwa siku moja ambapo sasa zitafanyika Novemba 10 mwaka huu. Mechi hizo ni Simba vs Toto Africans (Uwanja wa Taifa), Kagera Sugar vs Polisi Morogoro (Uwanja wa Kaitaba) na Oljoro JKT vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid).
Nyingine ni Tanzania Prisons vs JKT Ruvu (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine) na African Lyon vs Mtibwa Sugar (Azam Complex). Mechi ya Mgambo Shooting vs Azam (Azam Complex) yenyewe itachezwa Novemba 10 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa.
Nayo mechi ya Coastal Union vs Yanga (Uwanja wa Mkwakwani) itabaki Novemba 11 mwaka huu kwa vile Novemba 10 mwaka huu uwanja huo utakuwa na mechi nyingine. TFF imepanga utaratibu wa kuwapata kwa wakati wachezaji wa Yanga walioitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars.
Mabadiliko mengine ni ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ambapo mechi ya Villa Squad vs Transit Camp iliyokuwa ichezwe Novemba 8 mwaka huu sasa inachezwa Novemba 9 mwaka huu, na ile ya Novemba 7 mwaka huu kati ya Burkina Faso na Small Kids inachezwa Novemba 9 mwaka huu. Viwanja ni vilevile.

Saturday, October 27, 2012

0

YALIYOJIRI LIGI KUU TANZANIA BARA NA RATIBA YA MECHI ZIJAZO:: NA WENZETU SOKA IN BONGO

Posted in , , , ,

VPL: Simba yaipiga Azam, Yanga yaipiku Azam nafasi ya 2!!

Jumamosi, 27 Oktoba 2012 20:14
Chapisha Toleo la kuchapisha
VPL_LOGOKatika mfululizo wa Mechi za Ligi Kuu Vodacom, VPL, zilizochezwa leo, Mabingwa watetezi Simba wamefanikiwa kuichapa Azam bao 3-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuendelea kubaki kwenye uongozi huku Yanga, wakiwa huko Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha wakiifunga JKT Oljoro bao 1-0 na kuipokonya Azam nafasi ya Pili kwenye Msimamo wa Ligi.
++++++++++++++++++++++++++
MATOKEO/RATIBA:
Oktoba 27
Simba 3 Azam 1
JKT Oljoro 0 Yanga 1
African Lyon v Kagera Sugar
Mgambo JKT v Tanzania Prisons
Ruvu Shootings v Polisi Morogoro
++++++++++++++++++++++++++
Bao la ushindi la Yanga lilifungwa na Mbuyu Twite katika Dakika ya 53.
Katika Mechi ya Simba na Azam, John Bocco ndie alietangulia kuifungia Azam bao moja katika Dakika ya 5 lakini Simba ikazinduka na kupiga Bao 3 kupitia Felix Sunzu, Dakika ya 7, na bao mbili za Emmanuel Okwi.
++++++++++++++++++++++++++
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ