Next
Previous
Showing posts with label Mh. Jakaya Mrisho Kikwete. Show all posts

Sunday, August 4, 2013

0

MTANZANIA BINGWA WA KURUKA KAMBA DUNIANI APOKELEWA VYEMA NA RAISI KIKWETE

Posted in , , , ,
 Rais Kikwete akiwa na bingwa wa dunia Hamisi Mohamed pamoja na wachezaji wenzie na viongozi wa timu ya Tanzania iliyoshiriki katika mashindano ya dunia.
0

HAYA NDO MANENO ALIYOSEMA DK. SLAA DHIDI YA RAISI JAKAYA KIKWETE

Posted in , , ,
#NANUKUU
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli  yake ya  kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake ...


Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo.

Slaa  aliyasema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani  na hajachukua hatua dhidi ya wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi..."

"Alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda  na  badala  yake amempandisha cheo,” alisema Slaa.


Kauli  Dk Slaa imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kuwa Tanzania haina mgogoro na nchi ya Rwanda, kutokana na kauli za kejeli na matusi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa nchi hiyo dhidi yake na Tanzania.

Friday, August 2, 2013

0

PICHA ZA JINSI WASANII, MA-PRODUCER NA MA-PRESENTER WALIVYOKUA WAKIFUTURU NA MH. RAISI

Posted in ,

Wasanii mbali mbali na watangazaji walipata kualikwa ikulu jijini Dar, kwa ajili ya kuftari na Mh Raisi pamoja na familia yake.mara baada ya kuftari Mh Kikwete aliongea mawili matatu ikiwa ni pamoja na kuwapa moyo wasanii kwa kuendeleza sanaa maana hata yeye anapenda kusikiliza miziki yao


Tuesday, July 23, 2013

0

NAY WA MITEGO ASEMA ATAMPIGIA KAMPENI MH. LOWASSA 2015

Posted in , ,

Haya  ni  mashairi  aliyoyaandika Nay wa  mitego  kwenda  kwa  mtoto  wa  Rais  a.k.a Riz One  akimtaka  amwambie  baba  yake  kuwa  mtwara  hawataki  korosho, wanataka   gesi  na  pia Lowassa  asiache  kugombea  urais  maana  yupo  tayari  kumpigia  kampeni-2015


----------------
MASHAIRI YAKE:
Naongea na Riz one hey Riz One, we si mtoto wa raisi Riz one. Mwambie dingi yako Masela hawamuelewi wamakonde wa Mtwara hawataki tena Korosho, wanaitaka ges si mtawaua na mkong'oto?! Nani rafiki wa Lowasa anifikishie salam 2015 nataka agombee uraisi nitamfanyia kampeni wananchi wampe nafasi,
# Salam zao#
my new track coming soon.!!



Sunday, July 21, 2013

0

HII NDO ILE VIDEO AMBAYO RAISI KAGAME ALITOA KAULI NZITO JUU YA RAIS WETU JK.

Posted in ,

Thursday, July 11, 2013

0

OUR BUSY PRESIDENT: ONA SHUGHULI MBALIMBALI ANAZOZIFANYA RAISI J.M KIKWETE AKIWA IKULU

Posted in ,
 : Rais Jakaya Kikwete Mkurugenzi Mkuu wa  Irrigation System Ltd Bw. Choudhari Pramot baada ya maongezi naye leo Ikulu  jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana  na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es salaam

Friday, July 5, 2013

0

RAISI KIKWETE KUWA REFA MECHI YA WABUNGE (USIKU WA MATUMAINI)

Posted in ,


Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amekubali kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalo fanyika Jumapili hii, Julai 7 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Aidha, Rais atahutubia katika tamasha na pia atakuwa refa wa mechi za wabunge wa Yanga na Simba.
0

USIKU WA MATUMAINI: RAISI KIKWETE KUWA MGENI RASMI

Posted in , ,



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Matumaini ambalo litafanyika keshokutwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Mratibu wa tamasha hilo, Abdallah Mrisho, amesema Rais Kikwete ambaye hivi karibuni alikuwa na ugeni mkubwa wa Rais wa Marekani, Barack Obama, amekubali kuwa mgeni rasmi ambapo atatoa neno la matumaini kwa maelfu ya watu watakaojitokeza uwanjani hapo.
Akizungumzia zaidi juu ya ugeni huo mkubwa, Mrisho alisema: “Rais Kikwete amekubali ombi letu la kuwa mgeni rasmi, atatumia nafasi hiyo kutoa neno la matumaini kwa wote watakaojitokeza uwanjani hapo.
“Rais pia ndiye atakayefungua mechi ya Wabunge wa Simba dhidi ya Yanga ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa. Kama ujuavyo rais wetu ni mtu wa watu na ni mpenda michezo, hilo linajulikana siku zote.”

Aidha, Mrisho aliongeza kwa kusema kuwa shabaha ya tamasha hilo ni kuamsha upya imani ya Watanzania kwa nchi yao. Kuwafanya wawe wazalendo na kila mmoja kujiona analo jukumu la kufanya, kuhakikisha Tanzania yetu inapiga hatua.
“Mbali na Rais Kikwete, wengine watakaotoa neno la matumaini siku hiyo ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo.

Wednesday, May 8, 2013

0

HIZI NDO PICHA ZA RAISI KIKWETE AKIHANI MISIBA YA WALIOKUFA KATIKA MLIPUKO WA BOMU KANISA LA OLASITI

Posted in ,

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Bw. Joachim Assey (aliyekaa kushoto kwake) wakati akihani msiba wa msichana Patricia Joachim Assey (10) aliyefariki kutokana na mlipuko wa bomu jumapili iliyopita katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Parokia ya Olasiti jijini Arusha Mei 7, 2013.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ