Next
Previous
Showing posts with label Afande Sele. Show all posts

Monday, September 2, 2013

0

CHADEMA WAMKANA AFANDE SELE, HIKI NDO WALICHOKISEMA

Posted in ,


Gazeti la Habari Leo la siku ya leo tarehe 2 Septemba lenye kichwa cha habari "Chadema kuzoa wasanii mastaa" pamoja na mambo mengine, mwandishi amemnukuu mmoja wa wasanii toka mkoa wa Morogoro akisema amewahi kuombwa na viongozi wa mkoa wa CHADEMA kugombea Ubunge.

NAOMBA KUWEKA KUMBUKUMBU SAHIHI.
1. Mimi ndiye mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro, ninayeongoza Baraza la Uongoz la mkoa lenye wajumbe wa5 tu tangu mwaka 2009.
2. Katika vikao vyetu vyote hukujawahi kuwepo kwa AGENDA ya kumuomba/ kumshawishi mtu yeyote kugombea nafasi yoyote.

Tuesday, March 5, 2013

0

BRAND NEW TRACK: Afande Sele-Sukari

Posted in


Huu ni ujio mwingine kabisa kutoka kwa aliyewahi kuwa Mkali wa Rhymes, Afande Sele. Afande sasa amerudi tena na track yake mpya inayoitwa ''Sukari na Chai''.

Thursday, October 25, 2012

0

THE RETURN OF THE KING>> AFANDE SELE KUACHIA SONGI JIPYA PAMOJA NA VIDEO MBILI

Posted in
MSANII wa muziki wa Hip Hop kutoka mjini Morogoro Afande Sele, ameuambia mtandao wa DarTalk, kuwa anatarajia kutoa ngoma mpya inayokwenda kwa jina la ‘Soma Ule’, ngoma ambayo itakuwa ya tatu kuachia kwa mwaka huu ambayo itakuwa inazungumzia sana juu yaelimu.

Afande alisema kuwa kabla ya ngoma hiyo haijaenda sokoni ataachia kwanza video za ngoma zake mbili ambazo ni ‘Mr President’ na ‘Mashokoro Mangeni’, ambazo hazikufanya vizuri kwenye radio stations, anaamini kwenye upande wa televisheni zinaweza kufanya vizuri.

“Kwa sasa kuna goma yangu mpya ambayo natarajia kuachia lakini sina mpango wa kupeleka kazi yangu radioni, na ndiyo maana nataka kutoa video za ngoma zangu mbili,” alisema.

Saturday, May 5, 2012

0

Angalia Nyimbo 'MBONI YANGU-Tanzania All Stars for SAJUKI'

Posted in , , , , , , ,
Wasanii waungana Kumuimbia nyimbo Mboni Yangu kwa ajili ya Sajuki. Iangalie hii hapa. Umoja Ni NGUVU, Pamoja Tutafika na tutajenga Taifa lenye neema.
Kutoa Ni Moyo.
Madee
Kimodo na Barnaba
Ditto
Madee akirekodi sauti
Ditto,Amini na Afande Sele
Zamu ya Amini
Peter Msechu
Profesa Jay akiandika mistari yake
Afande Sele nae akiandaa mistari yake
Fid Q hakubakia

Friday, May 4, 2012

0

Wasanii na Wanasiasa waungana kutunga nyimbo ya kumsaidia Sajuki.

Posted in , , , , , , , , ,

Zaidi ya wasanii 25,baadhi ya watu maarufu,na wanasiasa vijana wakiwemo Zitto Kabwe, Halima Mdee, Esther Bulaya, Vicky Kamata na January Makamba wameshiriki katika wimbo,Mboni Yangu ,ambao umetungwa maalumu kwa ajili ya kuhamasisha michango kwa ajili ya msanii Sajuki.
Wimbo huo ambao umetengenezwa katika studio za THT pale Kinondoni jijini Dar-Es-Salaam chini ya produsa Tudd Thomas umefanywa maalum kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha za matibabu ya Sajuki ambaye anasumbuliwa na uvimbe ndani ya tumbo lake.
Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali vilvyokuwepo katika utengenezaji wa nyimbo hiyo Jumla ya wasanii 27 wanaofanya aina mbali mbali za muziki kama Bongo Fleva, Hip hop, Taarab na Afro Pop walishirikiana vizuri na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanikisha wimbo huo wa Mboni Yangu .
Nyimbo hiyo pia itakuwepo katika muvi ya msanii wastara ambaye ndiye ameshirikiana na Dina Marios wa kipindi cha Leo Tena Clouds Fm kwa pamoja walichagua jina la wimbo huo Mboni Yangu.Kwa mujibu wa Matangazo ya radio clouds asubuhi hii kwenye kipindi cha Teo Tena watu binafsi, ama kampuni au kikundi wanaweza kwenda mjengoni na kuchangia pesa kwa ajili ya matibabu ya msanii huyo ambayo yanatakiwa yakafanyike nchini India baadae mwezi huu.
Malengo ya ukusanyaji ambayo yamewekwa kwa siku ya leo ni angalau shilingi milioni 12.
Baadhi ya waliohusika katika nyimbo hiyo ni pamoja na Chidi Benz, Prof Jay, Ali kiba, Queen Darlin, WemaSepetu, Barnaba, Halima Mdee, Wastara, Mwasiti, Amini, Viki Kamata, Madee, afande Sele, Fid Q, Linex, William Mtitu na Wema Sepetu.
Tayari harambee ya kuchangisha pesa imeshaanza na kwa habari ambazo zimetangazwa mchangiaji wa kwanza ametoa dola 5000 na pia mkurugenzi wa Clouds Media Joseph Kusaga naye ametoa mchango wa Kiasi cha shilingi Milioni 1.

Credits to: bongo5.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ