Next
Previous
Showing posts with label Amini. Show all posts

Wednesday, November 27, 2013

0

NYIMBO MPYA: AMINI - USINIPE ROBO

Posted in ,
Amini

Wednesday, August 14, 2013

0

BARNABA NA AMINI WAANZISHA KUNDI JIPYA NJE YA THT

Posted in , ,
Wale wakali toka jumba la vipaji Tzee- THT walioishi kama pacha kwenye jumba hilo (Amini & Barnaba) wameungana na kuunda crew yao mpya kimziki iitwayo “GEMENIH” wakimaanisha wao ni kama mwezi na nyota angani. 


“Yap, Tumeungana kufanya kazi pamoja kama kundi nje ya THT tukiwa ni matunda ya THT na tumeamua kujiita hivyo kutokana na kutegemeana kwetu kwenye kazi na umuhimu wa uwepo wa kila mmoja kwenye mziki wa bongo kama umuhimu wa nyota na mwezi angani.” Barnaba alilidokeza BK.
Kundi hilo kwa sasa lina-bang hewani na ngoma yao ya ‘Why me’ huku wakiwa na mipango mingi ya utendaji wao wa kazi kama Gemenih. Pia waliongeza kitu juu ya Gemenih na THT.
“Kikubwa ni kwamba, watu wasidhani tumetoka au tuna ugomvi na THT ila tumehitimu mafunzo pale na kutunukiwa vyeti nasi ni matunda ya THT na bado tunashirikiana nao kwa kuwapa ushauri hata kuwatungia nyimbo. Kwa ufupi tumewaachia wengine nafasibaada ya sisi kufuzu mafunzo pale.” Amini aliongeza.
Gemenih ipo chini ya meneja aitwaye Moses Clemence ambaye ndiye ana-control mambo yote yahusuyo vijana hao.

Saturday, May 5, 2012

0

Angalia Nyimbo 'MBONI YANGU-Tanzania All Stars for SAJUKI'

Posted in , , , , , , ,
Wasanii waungana Kumuimbia nyimbo Mboni Yangu kwa ajili ya Sajuki. Iangalie hii hapa. Umoja Ni NGUVU, Pamoja Tutafika na tutajenga Taifa lenye neema.
Kutoa Ni Moyo.
Madee
Kimodo na Barnaba
Ditto
Madee akirekodi sauti
Ditto,Amini na Afande Sele
Zamu ya Amini
Peter Msechu
Profesa Jay akiandika mistari yake
Afande Sele nae akiandaa mistari yake
Fid Q hakubakia

Friday, May 4, 2012

0

Wasanii na Wanasiasa waungana kutunga nyimbo ya kumsaidia Sajuki.

Posted in , , , , , , , , ,

Zaidi ya wasanii 25,baadhi ya watu maarufu,na wanasiasa vijana wakiwemo Zitto Kabwe, Halima Mdee, Esther Bulaya, Vicky Kamata na January Makamba wameshiriki katika wimbo,Mboni Yangu ,ambao umetungwa maalumu kwa ajili ya kuhamasisha michango kwa ajili ya msanii Sajuki.
Wimbo huo ambao umetengenezwa katika studio za THT pale Kinondoni jijini Dar-Es-Salaam chini ya produsa Tudd Thomas umefanywa maalum kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha za matibabu ya Sajuki ambaye anasumbuliwa na uvimbe ndani ya tumbo lake.
Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali vilvyokuwepo katika utengenezaji wa nyimbo hiyo Jumla ya wasanii 27 wanaofanya aina mbali mbali za muziki kama Bongo Fleva, Hip hop, Taarab na Afro Pop walishirikiana vizuri na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanikisha wimbo huo wa Mboni Yangu .
Nyimbo hiyo pia itakuwepo katika muvi ya msanii wastara ambaye ndiye ameshirikiana na Dina Marios wa kipindi cha Leo Tena Clouds Fm kwa pamoja walichagua jina la wimbo huo Mboni Yangu.Kwa mujibu wa Matangazo ya radio clouds asubuhi hii kwenye kipindi cha Teo Tena watu binafsi, ama kampuni au kikundi wanaweza kwenda mjengoni na kuchangia pesa kwa ajili ya matibabu ya msanii huyo ambayo yanatakiwa yakafanyike nchini India baadae mwezi huu.
Malengo ya ukusanyaji ambayo yamewekwa kwa siku ya leo ni angalau shilingi milioni 12.
Baadhi ya waliohusika katika nyimbo hiyo ni pamoja na Chidi Benz, Prof Jay, Ali kiba, Queen Darlin, WemaSepetu, Barnaba, Halima Mdee, Wastara, Mwasiti, Amini, Viki Kamata, Madee, afande Sele, Fid Q, Linex, William Mtitu na Wema Sepetu.
Tayari harambee ya kuchangisha pesa imeshaanza na kwa habari ambazo zimetangazwa mchangiaji wa kwanza ametoa dola 5000 na pia mkurugenzi wa Clouds Media Joseph Kusaga naye ametoa mchango wa Kiasi cha shilingi Milioni 1.

Credits to: bongo5.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ