Next
Previous
Showing posts with label Ritah Poulsen. Show all posts

Friday, August 30, 2013

0

BIFU LA NAY WA MITEGO NA MADAM RITHA NI STORI ZA MTAANI: ANGALIA WAKIWA PAMOJA

Posted in , , ,

Takribani yapata wikii ya tatu baada ya Msanii
Nay wa Mitego kuachia kibao chake kinachotamba kama
Salamu zao....ndani ya nyimbo hiyo ametoa
kama kufikisha ujumbe kwa watu kadhaa,

Thursday, August 8, 2013

0

HIZI NDO SABABU ZILIZOMFANYA MADAM RITHA, AIHAMISHIE BSS TBC1

Posted in , , , , , , ,

Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 



Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.


“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1.


Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”

Sunday, September 30, 2012

0

KWANINI WASHINDI WA BSS HUFA BAADA YA MASHINDANO?

Posted in , ,
Leo wakati nakula chakula cha usiku nyumbani nikatumiwa text na mdogo wangu fulani hivi ambaye ndiye mmiliki wa Blogu Hii,Arnold Balati ''oya,cheki huyo mwanamke BSS anaimba nyimbo ya Adele'' basi bila hiyana nikachukua remote na kuweka ITV,yaani vitu nilivyovikuta huko ndani ni vya kusikitisha kwenye hili shindano wanaloita wenye Epic Bongo Star Search,hebu tujiulize kidogo ni mshindi gani wa Bongo Star Search unayemjua wewe anayekaribia hata robo ya msanii wa kawaida wa Tanzania,yaani mimi nawaona kama wanapotezewa muda wao..

Tujiulize washindi mbona hawasikiki baada ya mashindano kuisha,huwaga wanaenda wapi??lini mara ya mwisho umesikia ''ile nyimbo nzuri sana,yule ni mshindi wa BSS mwaka fulani''

Niwe mkweli tu,nimekuwa nikifuatilia mashindano makubwa kama X-Factor,American Idol na The Voice kwa kweli judges wana mchango mkubwa katika kumtengeneza au kumbomoa mshiriki/msanii

Kwetu Tanzania majaji wanaongoza kuharibu washiriki kwa asilimia 80,wanaoweza wanaamiwa hawajui  na wasioweza wanaambiwa ''wimbo mgumu ila wewe unaweza na ni staa'' Jamani!

Madam Rita= mfanyabiashara huyu anajua nini kuhusu music kama sio kutuharibia washiriki

Salama= Nilisema,Maisha Plus kunamuhitaji akaendeshe kipindi,sio jaji wa muziki huyu

Master J= ana akili ya kutengeneza beat na sio kujaji uwezo wa mshiriki


Kitime yuko wapi?Jay Dee anatakiwa,anaujua muziki na umemletea mafaniio ya kukubalika ndani na nje,AY je?  mbona hatuweki majaji wa maana???

Sina beef na mtu,ni mawazo yangu tu!!

EBSS BADILISHENI MAJAJI!!
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ