Next
Previous
Showing posts with label Dj Fetty. Show all posts

Tuesday, August 13, 2013

0

CHIDI BENZ AKIRI KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA NA KUWA AMEACHA

Posted in ,


DJ FETTY: Big up kwa Chidi Benzi leo hii amekiri kutumia madawa ya kulevya na kuachana nayo baada ya kutoka Nairobi kwa ajili ya matibabu...ameachia ngoma mpya pia pata time ya kuisikiliza ushauri jina la wimbo huo.

Monday, June 11, 2012

0

Africans Wamkubali DJ Fetty

Posted in , ,

Juzi Dj Fetty wa Tanzania ameithibitishia Afrika kuwa muziki anaujua, baada ya kuangusha ngoma za ukweli kwenye live show ya Big Brother.
Akiwa Dj wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kuwahi kupata heshima hiyo ya kuburudisha mamilioni ya watazamaji wa ukumbuni kwenye nyumba ya Big Brother pamoja na wale wanaoangalia kupitia TV, Fetty aliyekuwa anajiamini vya kutosha amepokea pongezi kutoka kwa wapenzi wa BBA barani kote.
Katika ukurasa rasmi wa Big Brother Afrika jana kumewekwa status iliyosema, “Our first lady DJ on the Big Brother stage…and she is trailblazing!”

Thursday, June 7, 2012

0

Dj Fetty kutinga Big Brother Stargame weekend hii

Posted in , , ,

Dj wa kwanza wa kike nchini Tanzania Fatma Hassan aka Dj Fetty wa Clouds Fm amepewa heshima ya kuwa Dj wa kwanza wa kike kutoka Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye mashindano ya Big Brother Africa.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook Fetty amesema, “Juma mosi hii na jumapili nitakua nikispin ndani ya Jumba la BBA STARGAME, nitume kwa kuniandikia playlist itakayo wapagawisha…na shinda very nice cape ya big brother na high quality Tshirt kutoka CloudsFm…legoooooo.”
Fetty ambaye kwa muda alikuwa amepumzika shughuli za udj na kuendelea na utangazaji wa kawaida, amesema imemlazimu kujifua tena ili kuhakikisha kuwa ‘haangushi maembe’ (kumix vibaya nyimbo) wakati atakapokuwa akipiga ngoma.
Amesema mwaliko huo ameupata katikati ya mwezi May na tangu hapo amekuwa akijikumbushia ujuzi kwenye ‘wheels of steel’ kwakuwa hiyo ni nafasi kubwa inayohitaji maandalizi ya kutosha.
Mwaka jana Dj wa kike kutoka kituo cha radio cha YFM cha Ghana Nana Kessewa Adu aka DJ Kess alialikwa pia kuburudisha kwenye Big Brother Amplified.
Hiyo si mara ya kwanza kwa Dj wa Clouds FM kupata mwaliko huo. Mwaka jana Dj Steve B naye alipewa fursa hiyo ya kuonesha ujuzi wa mikono yake kwenye 1 and 2!

 Source: bongo5.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ