Thursday, October 18, 2012

0

AVB KULIPA KISASI KWA CHELSEA??? NI KATIKA DABI YA LONDON JUMAMOSI. EPL YARUDI, RATIBA KAMILI.

Posted in , , , ,
Andre Villas-Boas, Meneja alietimuliwa kazi na Chelsea baada ya Miezi 9 tu mwanzoni mwa Mwaka huu, Jumamosi atapata nafasi safi ya kulipa kisasi wakati Timu yake anayoiongoza sasa Tottenham itakapoikaribisha Chelsea Uwanjani White Hart Lane katika Mechi ya Ligi Kuu England ambayo ni Dabi ya Jiji la London.
Msimu uliopita, Chelsea walimaliza Ligi wakiwa nafasi ya 6, nafasi mbili nyuma ya Tottenham lakini Chelsea wakaichukua nafasi ya Tottenham kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa vile Chelsea ndio Mabingwa watetezi wa Mashindano hayo na wao Tottenham kutupwa kucheza EUROPA LIGI.
Baada ya kutimuliwa Andre Villas-Boas, mwenye Miaka 34, nafasi yake huko Chelsea ikachukuliwa na aliekuwa Msaidizi wake, Roberto Di Matteo, ambae ndie aliiongoza Chelsea kutwaa Ubingwa wa Ulaya walipoitoa Bayern Munich kwa matuta Mwezi Mei kwenye Fainali huko Munich, Germany.
Chelsea watatinga White Hart Lane wakiwa ndio vinara wa Ligi wakiwa na Pointi 19 baada ya kushinda Mechi 6 na sare 1 na Tottenham wamepanda hadi nafasi ya 5 baada ya kuchinda Mechi zao 4 za mwisho ukiwemo ule ushindi wao murua huko Old Trafford walipoifunga Manchester United bao 3-2 huo ukiwa ushindi wao wa kwanza Uwanjani hapo katika Miaka 23.
Ikiwa Tottenham watamudu kuisimamisha Chelsea hilo litatoa mwanya kwa Timu zinazoifukuza Chelsea ambazo ni Manchester United, Mabingwa Manchester City na Everton.
Man United, ambao wako nafasi ya pili na wenye Pointi 15, wapo kwao Old Trafford kucheza na Stoke City, Man City, ambao pia wana Pointi 15, wapo ugenini kucheza na WBA ambao wako nafasi ya 6, na Everton, walio nafasi ya 4, wanacheza na Timu ya mkiani Queens Park Rangers.
Wachezaji toka Mechi za Kimataifa
Klabu nyingi za Ligi Kuu England zitakuwa zikisubiri kurudi kwa Wachezaji wao kutoka kuzichezea Nchi zao huku wakiwa na wasiwasi kama wako fiti lakini Chelsea watacheza na Spurs bila ya majeruhi Frank Lampard na Ryan Bertrand.
Manchester United, ambao wana listi ndefu ya majeruhi, wanaweza kupata ahueni baada ya Ashley Young na Chris Smalling kupona na kurejea mazoezini tangu Wiki iliyopita.
Man City wataenda huko Hawthorns kucheza na WBA bila ya David Villa ambae aliumia hivi juzi akiichezea Nchi yake Spain na pia Kiungo Jack Rodwell lakini machachari wao Mario Balotelli amepona na juzi alifunga bao wakati Nchi yake Italy ilipoichapa Denmark bao 3-1.
Arsenal, ambao wameteleza hadi nafasi ya 7 wakiwa na Pointi 12, watasafiri kwenda kucheza na Norwich City ambao Msimu huu hawajashinda hata Mechi moja ya Ligi.
Arsenal watacheza bila ya Theo Walcott  alieumizwa kifua kwenye Mechi ya Nchi yake England ilipocheza na San Marino Ijumaa iliyopita lakini Straika wao Olivier Giroud anaweza kucheza baada ya kuifungia Arsenal bao lake la kwanza kwenye Ligi Arsenal ilipoicharaza West Ham 3-1 katika Mechi iliyopita na pia kufunga bao muhimu kwa Nchi yake France ilipotoka 1-1 na Mabingwa wa Dunia Spain katika Mechi ya Kombe la Dunia juzi Jumanne.
RATIBA NA MAREFA wa MECHI za WIKIENDI:
Jumamosi Oktoba 20
Tottenham Hotspur v Chelsea
Refa: M Dean
Wasaidizi: S Ledger, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason
Fulham v Aston Villa
Refa: C Foy
Wasaidizi: M McDonough, D C Richards
Refa wa Akiba: I Williamson
Liverpool v Reading
Refa: R East
Wasaidizi: A Garratt, R West
Refa wa Akiba: K Friend
Manchester United v Stoke City
Refa: A Taylor
Wasaidizi: D Cann, S Long
Refa wa Akiba: M Halsey
Swansea City v Wigan Athletic
Refa: M Jones
Wasaidizi: H Lennard, A Halliday
Refa wa Akiba: K A Woolmer
West Bromwich Albion v Manchester City
Refa: M Clattenburg
Wasaidizi: S Beck, S Child
Refa wa Akiba: C Pawson
West Ham United v Southampton
Refa: N Swarbrick
Wasaidizi: J Collin, L Betts
Refa wa Akiba: J Moss
Norwich City v Arsenal
Refa: L Probert
Wasaidizi: R Ganfield, D Bryan
Refa wa Akiba: A Marriner
Jumapili Oktoba 21
Sunderland v Newcastle United
Refa: M Atkinson
Wasaidizi: M Mullarkey, S Burt
Refa wa Akiba: A Taylor
Queens Park Rangers v Everton
Refa: J Moss
Wasaidizi: J Flynn, C Breakspear
Refa wa Akiba: P. Dowd

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ