KOMBE LA MABARA 2013 | CONFEDERATIONS CUP 2013 NCHINI BRAZILI KUANZA KESHO
Posted in Brazil, FIFA Confederations Cup, Fifa World Cup 2014, Japan, World Cup 2014 BrazilIFUATAYO NI TATHMINI YA MECHI HII YA UFUNGUZI!
Hali za Wachezaji
Brazil wanatarajiwa kutumia Mfumo wa 4-2-3-1 huku Staa wao Neymar akicheza nyuma ya Straika Fred na langoni kuwepo Kipa Julio Cesar ingawa Kocha Luiz Felipe Scolari atalazimika kuamua nani aanze Fulbeki ya kushoto kati ya Marcelo au Filipe Luis.
Japan wanaweza kumkosa Mchezeshaji wao mkubwa Keisuke Honda na hilo linaweza kumfanya Shinji Kagawa akacheza kama Kiungo wa kati badala ya Kiungo wa pembeni kama anavyochezeshwa akiwa na Japan.
Nahodha wa Japan Makoto Hasebe atarudi tena dimbani baada ya kutumikia Kifungo cha Mechi moja.
Tathmini ya Mechi
Hiki ndio ‘Kipima Joto’ rasmi kwa Brazil kuweza kuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia Mwakani na pia kama wataweza tena kurudia utawala wao wa Kombe la Dunia kwani wao ndio Nchi iliyotwaa Kombe hilo mara nyingi walipolichukua mara 5.
Brazil, kama Wenyeji wapo Fainali hizo za Kombe la Dunia, na Wiki iliyopita Japan ilikuwa Nchi ya kwanza Duniani kuungana nao kwenye Fainali hizo baada ya kufuzu kutoka Kanda ya Bara la Asia.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++
GLT==TEKNOLOJIA YA MSTARINI GOLINI KUTUMIKA:












