>>MECHI YA GERRARD; LIVERPOOL v OLYMPIAKOS, ANFIELD AGOSTI 3!
>>RIO MKATABA MPYA, SCHOLES KUSTAAFU!!

NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard, ili kumtukuza, atachezewa Mechi maalumUwanjani Anfield na huko Old Trafford, Mabingwa wapya wa England, Manchester United, wamedokeza kuwa Beki wao Rio Ferdinand atasaini Mkataba mpya.
STEVEN GERRARD: KUENZIWA KWA MECHI MAALUM!
Liverpool wametangaza kuwa Nahodha wao Steven Gerrard, Miaka 32, atatukuzwa kwa kuwekewa Mechi maalum hapo Agosti 3 Uwanjani Anfield Liverpool watakapocheza na Olympiakos ya Ugiriki.
Pesa zitakazoingizwa kwenye Mechi hiyo zitakwenda kwenye Mfuko wa Hisani wa Steven Gerrard.
Gerrard ameichezea Liverpool Mechi 439 za Ligi tangu Novemba 1998.
+++++++++++++++++++++++
GERRARD-Historia:
-Mechi 628 kuichezea Liverpool
-Mabao 159 kwa Liverpool
-Mataji:
=1 Champions League

=1 Uefa Cup
=2 FA Cup
=2 Kombe la Ligi
+++++++++++++++++++++++
Hapo Tarehe 29 Novemba 1998, Steven Gerrard aliichezea Liverpool Mechi yake ya kwanza kwenye BPL, Barclays Premier League, dhidi ya Blackburn Rovers.
Mwaka 2003, Steven Gerrard alimrithi Sami Hyypia na kuwa Nahodha wa Liverpool.
Katika Misimu ya 2004-05, 2005-06 na 2008-09, Gerrard ndie alikuwa Mfungaji Bora wa Klabu ambae ameifungia Jumla ya Mabao 159 katika Mechi 628.
Mkataba wa sasa wa Gerrard unamalizika mwishoni mwa Msimu wa 2013/14.
RIO FERDINAND KUPEWA MKATABA MPYA MANCHESTER UNITED