Monday, September 10, 2012

0

Bifu La John Teery na Anton Ferdinand Kuendelea Jumamosi??

Posted in , , ,
>>KUCHEZWA Septemba 15, SWALI Wachezaji watapeana mikono??
Ipo minong’ono John Terry hatapewa mkono na  Anton Ferdinand wakati Timu hizi zitakapokutana Jumamosi Septemba 15 katika Mechi ya Ligi Kuu England Uwanjani Loftus Road.
Hadi sasa Ligi Kuu haijatoa tamko kama itazuia ile desturi ya Timu kupeana mikono kabla ya Mechi kama ilivyofanya mara ya mwisho Timu hizi kukutana Mwezi Aprili ili kuepusha shari kati ya Nahodha wa Chelsea John Terry na Beki wa QPR Antoin Ferdinand ambao walikwaruzana kwenye Mechi Uwanja wa Loftus Road Mwezi Oktoba Mwaka jana na hatimae Terry akafikishwa Mahakamani na kushitakiwa kwa kukashifu kibaguzi lakini akashinda Kesi hiyo.
FERDINAND_v_TERRYMara baada ya uamuzi wa Mahakama, Chama cha Soka England, FA, kiliamua kufufua uchunguzi wake kuhusu tukio hilo na hatimae kuamua kumshitaki Terry kwa utovu wa nidhamu na kukashifu kibaguzi.
Wakati FA ikiwa bado haijatoa hukumu yake dhidi ya Terry, inasadikika bado ipo mikwaruzo kati ya Wachezaji hao na ndio maana Wadau wanaifuatilia sana Mechi ya QPR na Chelsea Jumamosi ijayo.
Mwishoni mwa Mwezi huu, Terry anatarajiwa kwenda mbele ya Jopo maalum la Chama cha Soka England, FA, ili kujitetea binafsi katika Kesi hiyo yake inayomuhusu Ferdinand baada ya yeye mwenyewe kuomba kufika mwenyewe mbele ya Jopo la FA ili kutoa utetezi wake.
Baada ya tukio kwenye Mechi hiyo ya Oktoba Mwaka jana, QPR na Chelsea zimeshakutana mara mbili, Mwezi Januari kwenye FA Cup na Aprili kwenye Ligi, na mara zote hizo kupeana mikono kabla ya Mechi kulifutwa ili kusichochee ugomvi zaidi.
Safari hii, Ligi Kuu inasemekana itafuta utaratibu wa kupeana mikono ikiwa tu itaombwa na moja ya Klabu hizo mbili.
CHANZO: Soka In Bongo

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ