Wednesday, May 23, 2012

0

TFF yapinga ‘Mapinduzi’ Yanga!

Posted in ,

YANGASHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limetangaza kutoutambaua uongozi wa muda uliowekwa madarakani na Wanachama wa Yanga. 
Majuzi, zaidi ya wanachama 600 wa Yanga wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Yanga, Bakili Makele, pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee, Ibrahim Akilimali, walitangaza kumng’oa madarakani Mwenyekiti wao, Lloyd Nchunga.
Jana TFF imesambaza Taarifa iliyosainiwa na Katibu Mkuu wake, Angetile Osiah, ikitaka Wananachama wao kufuata Katiba zao zinavyosema kuhusu utaratibu mzima wa uongozi na namna ya kuwaondoa viongozi wao madarakani. 
Osiah alisema hakuna Katiba yoyote inayomlinda kiongozi aendelee kukaa madarakani, lakini Klabu zinapaswa kufuata utashi wa Katiba zao zinavyosema ili kufanya mabadiliko ya uongozi ndani ya vyama vyao na si kupitia Vikao visivyo halali. 
TFF imesema haiko tayari kufanya kazi na uongozi wa Kamati za muda na imewaonya Wanachama wa TFF kuwa lazima waheshimu Katiba zao katika kufikia maamuzi mbalimbali wanayofanya. 
Kuhusu kujiuzulu Wajumbe wa Kamati ya Utendaji wa Klabu hiyo, Osiah alifafanua kuwa Katiba ya Yanga inasema wazi kuwa lazima nafasi za Wajumbe hao kujazwa kwenye Mkutano Mkuu wa Klabu hiyo uliopangwa kufanyika Julai 15. 
Tayari wajumbe saba kati ya 13 wa Kamati ya Utendaji ya Yanga wamejiuzulu na mmoja, Theonist Rutashoborwa, amefariki dunia Mwezi uliopita. 
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ambao hawajajiuzulu ni Mwenyekiti Nchunga, Sarah Ramadhani, Charles Mngodo, Salum Rupia na Tito Ossoro.

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ