KUTOKA TFF NA WENZETU SOKAinBONGO.com>> RATIBA YAREKEBISHWA KUPISHA MECHI YA STARS
Posted in Harambee Stars, Taifa Stars, TFF, Vodacom Premier League
>> UCHAGUZI TAREFA, TAFCA SASA DESEMBA 22
>> TFF YATOA PONGEZI KWA UONGOZI MPYA FA MWANZA
Kamati
ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF, imefanya
mabadiliko madogo ya ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom, VPL, ili kupitisha
Mechi ya Kirafiki ya Kalenda ya FIFA kati ya Taifa Stars na Kenya,
Harambe Stars, itakayochezwa Novemba 14 Jijini Mwanza na mabadiliko
mengine yanahusu Ratiba ya Ligi Daraja la Kwanza, FDL.
Zifuatazo ni Taarifa kamili za TFF:
Release No. 180
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Novemba 9, 2012
MECHI TANO VPL ZAPISHA TAIFA STARS
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) imefanya mabadiliko madogo ya ratiba ya Ligi Kuu
ya Vodacom ili kupitisha mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kati ya Taifa Stars na Kenya (Harambe
Stars) itakayochezwa Novemba 14 mwaka huu jijini Mwanza.
Mechi tano za ligi hiyo zilizokuwa
zichezwe Novemba 11 mwaka huu, zimerejeshwa nyuma kwa siku moja ambapo
sasa zitafanyika Novemba 10 mwaka huu. Mechi hizo ni Simba vs Toto
Africans (Uwanja wa Taifa), Kagera Sugar vs Polisi Morogoro (Uwanja wa
Kaitaba) na Oljoro JKT vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh
Kaluta Amri Abeid).
Nyingine ni Tanzania Prisons vs JKT Ruvu
(Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine) na African Lyon vs Mtibwa Sugar (Azam
Complex). Mechi ya Mgambo Shooting vs Azam (Azam Complex) yenyewe
itachezwa Novemba 10 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa.
Nayo mechi ya Coastal Union vs Yanga
(Uwanja wa Mkwakwani) itabaki Novemba 11 mwaka huu kwa vile Novemba 10
mwaka huu uwanja huo utakuwa na mechi nyingine. TFF imepanga utaratibu
wa kuwapata kwa wakati wachezaji wa Yanga walioitwa kwenye kikosi cha
Taifa Stars.
Mabadiliko mengine ni ya Ligi Daraja la
Kwanza (FDL) ambapo mechi ya Villa Squad vs Transit Camp iliyokuwa
ichezwe Novemba 8 mwaka huu sasa inachezwa Novemba 9 mwaka huu, na ile
ya Novemba 7 mwaka huu kati ya Burkina Faso na Small Kids inachezwa
Novemba 9 mwaka huu. Viwanja ni vilevile.
Kamati ya Ligi imelazimika kufanya
mabadiliko hayo kutokana na viwanja husika kuwa na mechi nyingine, na
vilevile Small Kids kupata matatizo ya usafiri kutoka mkoani Rukwa
kwenda Morogoro.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Release No. 181
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Novemba 9, 2012
UCHAGUZI TAREFA, TAFCA SASA DESEMBA 22
Uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Mpira
wa Miguu Mkoa wa Tabora (TAREFA) na Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu
Tanzania (TAFCA) sasa utafanyika Desemba 22 mwaka huu.
Kwa mujibu wa ratiba za uchaguzi za
vyama hivyo, Kamati zao za uchaguzi zitatangaza kuanza mchakato wa
uchaguzi Novemba 10 mwaka huu wakati fomu kwa wanaotaka kugombea uongozi
zitaanza kutolewa Novemba 12 mwaka huu. Mwisho wa kuchukua na kurudisha
fomu ni Novemba 16 mwaka huu.
Kamati ya Uchaguzi ya Shirkisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa mwongozo huo kwa Kamati ya Uchaguzi ya
TAFCA baada ya kuomba hivyo kutokana na wagombea sita tu kujitokeza
kuomba nafasi tatu za uongozi katika mchakato wa awali.
Kwa waombaji ambao awali walichukua na
kulipia ada ya fomu za kugombea uongozi TAFCA na TAREFA, hawatatakiwa
kulipia tena ada kwa nafasi zile zile walizoomba, isipokuwa watatakiwa
kujaza fomu upya.
PONGEZI KWA UONGOZI MPYA FA MWANZA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa
wa Mwanza (MZFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika Novemba 8
mwaka huu.
Ushindi waliopata viongozi
waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano
Mkuu wa MZFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo
katika Mkoa wa Mwanza.
TFF inaahidi kutoa ushirikiano wa
kutosha kwa Kamati za Utendaji ya MZFA iliyochaguliwa chini ya uenyekiti
wa Patrick Songora aliyechaguliwa kwa kipindi cha pili mfululizo.
Uongozi huo mpya wa MZFA una changamoto
nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu
kwa kuzingatia katiba ya chama chao pamoja na vyombo vya mpira wa miguu
vilivyo juu yao.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya
Uchaguzi ya MZFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi
unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa kuongoza MZFA ni
Patrick Songora (Mwenyekiti), Nassoro Mabrouk (Katibu) na Richard
Kadutu (Mwakilishi wa Klabu TFF).
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
0 Maoni/comments: