Saturday, October 27, 2012

0

NI CHELSEA VS MANCHESTER UNITED HAPO KESHO, LIVERPOOL NA EVERTON!!!

Posted in , ,
>>JUMAPILI DABI ya LIVERPOOL ya 219: Everton v Liverpool!
>>KAGAWA nje WIKI 4!!
>>JUA MAREFA wa KILA MECHI!!
Timu zote 20 za Ligi Kuu England zitashuka dimbani kwa Mechi za Ligi Jumamosi na Jumapili kwa kucheza Mechi 10 lakini kati ya hizo, bila shaka, BIGI MECHI itakuwa ile ya Stamford Bridge ambayo vinara wa Ligi Chelsea wataivaa Manchester United iliyo nafasi ya pili na Mechi ya mvuto ni ile DABI ya Jiji la Liverpool Uwanjani Goodison Park kati ya Everton na Liverpool.
++++++++++++++++++++++
Lakini, Manchester United watatinga huko Stamford Bridge huku wakiwa na habari mbaya za kumkosa Kiungo wao mahiri kutoka Japan, Shinji Kagawa, ambae atalazimika kuwa nje ya Uwanja kwa Wiki 3 hadi 4 akiuguza goti aliloumia kwenye Mechi na Braga iliyochezwa majuzi Jumanne.
Wakati, Sir Alex Ferguson anathibitisha kukosekana kwa Kagawa pia alithibitisha kurudi tena Uwanjani kwa Chris Smalling ambae alivunjika kidole cha mguu.
Msimu huu, Chelsea wamepoteza Pointi 2 tu kwenye Ligi  na hawajafungwa hata Mechi moja na wako Pointi 4 mbele ya Man United na wakiwa na Wachezaji hatari Eden Hazard, Juan Mata na Oscar wamekuwa tishio katika mashambulizi yao.
Hilo linatambulika kwa Ferguson ambae amesema: “Siku zote ni gemu ngumu kwa Chelsea na Man United. Unazo Timu nzuri. Wote wapo juu baada ya kuanza vyema na Chelsea wanatumia mfumo wa kuvutia na hilo lazima tulikabili. Wamewaleta Oscar na Hazard ni Wachezaji wazuri. Wamemwingiza Mata ambae anafana uchezaji na kina Oscar ambao wanacheza nyuma tu ya Straika wao mmoja. Si mfumo rahisi kuukabili lakini lazima tutafute njia. Kwa sasa hawana Drogba tena na wamebidi wabadilike. Walipokuwa na Drogba walikuwa wanaweza kucheza mipira mirefu au kupitia kati. Sasa hayupo, ni moja kwa moja wanapitisha mipira kupitia kati kwenye Kiungo.”
DABI: Everton v Liverpool
Tangu enzi hii ni mojawapo ya Dabi inayoheshimika Duniani yenye ushindani mkali na hii ni Dabi ya 219 ambapo Liverpool wameshinda mara 87, Everton mara 66 na sare 65.
Katika Mechi 11 za Ligi Kuu ambazo Everton wamekutana na Liverpool wameshinda Mechi 1 tu, sare 3 na kufungwa 7.
Lakini, safari hii, Everton watajiona kama wana nafasi kubwa kuifunga Liverpool hasa kwa vile wao wameanza Msimu vizuri na wapo nafasi ya 4 kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa na Pointi 15 huku Liverpool wakiwa nafasi ya 12 na wana Pointi 9 tu.





Jumapili Oktoba 28
Everton v Liverpool
Refa: A Marriner
Refa Wasaidizi: S Ledger, S Bennett
Refa wa Akiba: P Dowd
Newcastle United v West Bromwich Albion
Refa: C Foy
Refa Wasaidizi: H Lennard, R West
Refa wa Akiba: M Halsey
Southampton v Tottenham Hotspur
Refa: L Mason
Refa Wasaidizi: D England, D C Richards
Refa wa Akiba: R East
Chelsea v Manchester United
Refa: M Clattenburg
Refa Wasaidizi: M McDonough, S Long
Refa wa Akiba: M Jones

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ