Friday, July 6, 2012

0

NANI KASEMA SUPERSTARS WANARIDHIKA NA PESA??RIHANNA AWAFUNGULIA KESI YA MADAI FORMER ACCOUNTANTS(wapiga mahesabu wake wa zamani) KWA UPOTEVU WA MAMILIONI YA DOLLAR

Posted in , , ,
Rihanna kafungua rasmi kesi ya dhidi ya wahasibu wake wa zamani kwa upotevu wa mailioni ya dola(sio shilingi).
Muimbaji huyo aliyetokea kutamba na ngoma kama Pon de Replay,Music of the sun,Unfaithful na nyinginezo nyingi ameamua kufungua kesi hiyo mnamo jana (5 July) huku akiwatuhumu kwa kushindwa kumshauri apunguze matumizi katika ziara yake ya ''The last girl on earth'' ya mwaka 2009,Rihanna amenena kuwa ziara hiyo ilikuwa na hasara za kutisha huku accountants hao wakiinigiza mfukoni 22% ya pesa na yeye kuambulia 6% ya pesa yote.


Rihanna aliitema kampuni hiyo ya mahesabu September 2010 na amekiri tangu kuachana nao faida za tour zake na music zimeongezea kwa zaidi ya 40%.
Mwaka jana Rihanna aliifungulia pia shitaka kampuni ya kuuza nyumba ya Los Angeles Real Estate kwa madai ya kuwa imekula pesa nyingi zaidi ya kiasi halali kwenye manunuzi ya moja ya nyumba zake huko L.A.
Mchungulie Rihanna wa kipindi kileeeee alivyotoka hapa chini



Habari hii imeletwa kwenu kwa hisani ya Digital Spy Uk.

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ