CHUO KIKUU CHALEA MAKAHABA: NI CHUO KIKUU DODOMA AMBACHO KIMEENDELEA TAWALIWA NA HAWA MADADA POA
Posted in Malaya, UDOM
Ongezeko la makahaba mjini Dodoma limeendelea kuwa kero kwa chuo kikuu cha Dodoma na wanafunzi wake kwa ujumla....
Kero hiyo imekuwa ikisababishwa na baadhi ya makahaba hao kujifanya wanafunzi wa chuo hicho kwa lengo la kujiimarisha kibiashara...
Takribani miezi mitatu iliyopita, kahaba mmoja alinasawa na polisi mjini Dodoma akijiuza kwa kujinadi kuwa yeye ni mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu cha Dodoma ..
Baada ya mahojiano ya kina na Polisi Central, ilibainika kuwa kahaba huyo hakuwa Mtanzania na hakuwa mwanafunzi wa chuo chochote hapa nchini na badala yake alikuwa ni raia wa Malawi.
Upekuzi wa polisi ulifanikiwa kunasa ARVs za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI toka kwa mwanamke huyo aliyekuwa akiendesha maisha yake kwa kuuza mwili wake maeneo ya Uhindini mkoani humo.
Mbali na ushahidi huo, mtandao huu umefanikiwa kumnasa binti mwingine anayejiita SECHE MAUTAMU...












