Next
Previous
Showing posts with label Keko. Show all posts

Wednesday, September 5, 2012

0

LINEX Kufanya Ngoma na KEKO&AVRIL

Posted in , ,

MSANII anayetamba na ngoma ya ‘Aifola’, Linex ameuambia mtandao wa DarTalk kuwa anatarajia kufanya ngoma ya kipekee kabisa na wasanii maarufu kutoka Afrika Mashariki, Avril kutoka Kenya na Keko kutoka Uganda ngoma inayokwenda kwa jina ‘Wema kwa Ubaya’.

Avril kwa anatamba na ngoma ‘Kitu Kimoja’, ambapo pia aliwahi kutamba zaidi na ngoma yake ya ‘Chokoza’, huku kwa Keko ambaye bado anatamba na ‘Make You Dance’.

Akizungumzia ishu hiyo kubwa ambayo haijafanywa na msanii wa Tanzania kufanya ngoma na nyota hao wanaokuja juu, alidai kuwa anafikilia kuwa afanye nao kazi moja moja au ya pamoja lakini anaamini kazi hiyo ya pamoja itakuwa nzuri.

“Ishu kubwa ambayo ipo kwa sasa ni kufanya ngoma na wasanii hao kutoka Kenya na Uganda, na baada ya hapo bado ratiba nyingine zitaendelea kama kawa,” alisema.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ