Monday, August 13, 2012

0

Tanzania Isiyo Na Medali Za Olympic

Posted in
Kazi mliyotutuma kwa kweli ilikuwa ngumu sana..japo tulifanya mazoezi kabla ila hapana aisee!
1.Kwenye SWIMMING,yale maji yao yalikuwa ya moto kweli,kushinda hata ya Coco beach tulipofanyia mazoezi,maji utasema uko bafuni unaoga halafu marumaru zile zinapendeza hadi zinachanganya
2.Kwenye MARATHON,barabara zao zina mikunjo mingi sana kama za Kampala na Nairobi ndo maana Kenya na Uganda walishinda..sisi tumezoea za one way kama Mwenge-Posta
3.Kwenye BOXING,wale watu wao wana sura za kitoto na warembo sana hadi unaogopa kuwapiga unaweza kupata kesi

Yasingekua hayo mambo tuliyoyataja tungerudi na Gold kwenye michezo yote!Ikitokea ya nchi nyingine msisite kutuita tukajaribu tena!!

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ