Serikali Yaamua Kuchangia Matibabu Ya Sajuki
Posted in Sajuki
Kutokana na hali ya Msanii Sadick Juma Kiwolo au maarufu kama Sajuki
kuendelea kuwa mbaya serikali imeamua kuingilia kati swala hilo na
kuchukua uamuzi wa kumsaidia kimatibabu msanii huyo hadi pale atakapo
pata nafuu. Sajuki ambaye kwa sasa amelazwa katika hospitali ya Muhimbili na amegundulika kuwa anatatizo la kufeli kwa Figo na kwamba yuko chini ya uangalizi na uchunguzi zaidi. Katibu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Wilson Makubi amesema kuwa serikali imejitolea kumsafirisha msanii huyo kwa gharama zote pamoja na gharama za matibabu akiwa nchini India. Sajuki anatariwa kusafiri wiki ijayo baada ya taratibu zote zitakapo kamilika.
0 Maoni/comments: