Monday, December 17, 2012

0

MTUKUTU BALLOTELI AISHTAKI MAN-CITY

Posted in ,
Kutoka SokaInBongo.com
Straika wa Manchester City, mwenye vituko bwelele, Mario Balotelli, ameamua kuifikisha Klabu yake mbele ya Baraza Maalum la Ligi Kuu England akipinga kupigwa Faini ya Mshahara wa Wiki mbili kwa rekodi yake mbovu ya utovu wake wa Nidhamu.
BALOTELLI-WHY_ALWAYS_MEBalotelli, mwenye Miaka 22, ameshazikosa Mechi 11 za Man City kwa Msimu uliopita akiwa anatumikia Vifungo mbalimbali alivyopewa kwa makosa mbalimbali.
Mara baada ya Balotelli kutwangwa Faini na Man City alikata Rufaa mbele ya Jopo Huru la Klabu hiyo lakini Rufaa yake ilitupiliwa mbali na sasa ameamua kufikisha Rufaa yake kwenye Baraza Maalum la Ligi Kuu England.
Balotelli anatarajiwa kuwepo mwenyewe kwenye Rufaa yake mbele ya Baraza hilo akitetewa na Mwanasheria wake kutoka Italy pamoja na Mwakilishi wa PFA [Professional Footballers' Association], Chama cha Wachezaji wa Kulipwa.
+++++++++++++++++++++
VIFUNGO vya BALOTELLI 2011/12:
-v Dynamo Kiev (Machi 2011): Alitolewa nje kwa Rafu mbaya dhidi ya Goran Popov. Alifungiwa Mechi 4 za UEFA CHAMPIONZ LIGI.
-v Spurs (Januari 2012): Alifungiwa Mechi 4 na FA baada ya kumtimba  Scott Parker bila Refa kuona.
-v Arsenal (Aprili 2012): Alitolewa nje baada ya kulambwa Kadi za Njano mbili ikiwemo Rafu mbaya kwa Alex Song. Alifungiwa Mechi 3.
+++++++++++++++++++++
Rufaa hii ya Balotelli inashangaza maana Klabu zinaruhusiwa kumpiga Faini Mchezaji wake hadi kufikia Mishahara ya Wiki mbili lakini zaidi ya hapo inabidi wapeleke Kesi kwa Baraza Maalum la Ligi Kuu England ili wapewe Kibali.
Hatua hii ya Balotelli pia inastajabisha maana kawaida Klabu na Mchezaji wake humalizana wenyewe ndani ya Klabu yao lakini Kesi hii, ambayo Man City waliifungua tangu Aprili 2012, imeshindikana licha ya PFA kujaribu kuisuluhisha.
Katika kipindi hicho kilichotajwa cha utovu wa Nidhamu wa Balotelli alipewa jumla ya Kadi za Njano 9 na Kadi Nyekundu 3.
Katika Mechi yake ya mwisho na Man City, Balotelli alitolewa mapema Kipindi cha Pili wakati Man City walipochapwa 3-2 na Man United hapo Desemba 9 Uwanjani Etihad na Mechi iliyofuatia, juzi Jumamosi, Man City walipoifunga 3-1 Newcastle, Balotelli hakuwemo kabisa kwenye Kikosi.
Mara baada ya Mechi hiyo na Newcastle, Meneja wa Man City Roberto Mancini alisema: “Wakati huu, Mario hayupo kwenye fomu nzuri na ndio maana yuko nyumbani. Ni sababu hiyo tu. Kurudi tena kwenye Timu ni lazima afanye bidii mazoezini na akichezeshwa lazima acheze vizuri.”

0 Maoni/comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Msimamo Ligi Kuu TZ